07 October, 2012

TANGAZA BIASHARA YAKO KIMATAIFA BURE!!!


Ukitaka tangaza biashara yako bure mcheki mdau kama anavo eleza hapa chini
Website http://www.absolutelyawesomethings.com/   inayomilikiwa na kuandikwa na Mtanzania hapa Newyork inatoa offer kwa Mtanzania mahali popote alipo duniani kutangaza biashara/sanaa yake katika website hiyo. Matangazo yatawekwa kwenye website kwa muda wa mwezi mzima, kuanzia  leo tarehe 5/10/2012 mpaka 5/11/2012. Kama wewe ni Mtanzania  na

1. unaduka lililosajiliwa online na unapenda kuitangaza biashara yako au

2. una sanaa ambayo unaifanya mwenye ungependa

 kuitangaza kimataifa.
 wasiliana nami kwa email sophie@absolutelyawesomethings.com.
Hii ni  kutoa shukrani na vilevile kuwapromote wazawa kimataifa kwa juhudi zao wanazozifanya.

04 August, 2012

KISA CHA MSICHANA ALIYESAMBAZA UKIMWI MAKUSUDI

Nimeona si vibaya wasomaji wangu mkaipata hii habari japo imepita muda lakini HIV/AIDS bado tunayo katika jamii na mtu kama huyu ni mfano tu.Ni wazi kua japo ni siri kubwa lakini kuna watu wenye magonjwa kama huyu dada wanaojua ni wagonjwa (mabibi kwa mabwana) wanaambukiza wengine kwa maksudi.Baadhi yetu tunawajua ila tuna kaa kimya na kuona kama haituhusu, lakini ukweli ni kwamba inatuhusu sana maana ile ni 'chain' tu hata wewe unaweza pata UKIMWI kupitia mtu huyohuyo unaysema hakuhusu.Naomba nieleweke kua wale wanaowajua wathirika na wanasambaza virusi vya 'UKIMWI'  kwa makusudi walipotiwe kwenye vyombo vya dola ili wachukuliwe hatua za kisheria kwani si ustarabu.


Kusoma kisa kilichonifanya niandike haya  bofya HAPA

ETI MBONA HUKUI KULIKONI?


04 June, 2012

Latest News - Diesel Vs Petrol


Diesel engines used to be noisy, smelly and somewhat agricultural. Then car makers wised up, made the engines cleaner, more powerful and refined, and with diesel cheaper than petrol at the pumps, the fuel suddenly became more viable. Not for long. With the Chancellor making diesel pricier than petrol, choosing between the two fuel forms is now no longer as clear cut.

If it was purely down to miles per gallon, diesel would win. Easily. A Ford Fiesta 1.4 TDCi returns a quoted Combined consumption of 69mpg. The petrol equivalent of the same capacity does 49mpg.

But petrol hits back with the model’s purchase-price advantage. The petrol Fiesta in three-door Edge trim would set you back £12,195. The diesel version costs £12,995. And the difference isn’t going to get smaller. Ford Powertrain’s director Andrew Fraser explains: “Diesel engines are getting more expensive to build due to increased legislation. Last year a diesel particulate filter (DPF) had to be fitted, which required an injection upgrade. In 2015, they’ll have to abide by Euro VI emissions standards, so most diesel engines will need a Nitrogen Oxide trap. It’ll all add up to making the payback period for diesel longer.”

The addition of DPFs in particular has been contentious. Vanessa Guyll from the AA’s technical services says: “The DPF and exhaust gas recirculation mean diesels really aren’t viable for short journeys and town work. The DPF doesn’t get hot enough to clear itself out. We get called to about 700 breakdowns a month for blocked DPFs.

“For anyone who potters around town and doesn’t do journeys that are a minimum of 10 miles we wouldn’t advise a diesel. Any savings owners might make on road tax would be quickly wiped out by fixing problems with the emissions equipment if usage isn’t suitable.”



 Wewe unasemaje?

28 April, 2012

MATANGAZO YALIYOSHAMIRI MAGAZETINI NA KWENYE MABANGO MITAANI


                                            Eti mafanikio siku 3, hivi hii imekaaje?

19 April, 2012

MZEE WA VIJISENTI WA NIGERIA AFUNGWA MIAKA 13

Gavana wa zamani wa moja ya majimbo tajiri Nigeria, (Delta State) bwana James Ibori afungwa miaka 13 jela.Bwana Ibori alikamatwa mwaka 2010 Dubai kwa makosa ya kujipatia mamilioni kwa njia ya udanganyifu.Mheshimiwa huyo wa ugavana jimbo tajwa kwa miaka ya 1997-2007 baada ya kukamatwa alipelekwa nchini Uingereza ambako alikua ameweka baadhi ya pesa na kununua majumba ya kifahari kwa mahojiano zaidi na polisi mpaka kufikia uamuzi huo wa kufungwa miaka 13 baada ya kuthibitika.Sambamba na hilo mheshimiwa atafilisiwa kwa maslahi ya taifa hilo kubwa kabisa balani Afrika,hususani Afrika Magharibi.


Jeshi la polisi nchini Uingereza lilishangazwa na manunuzi ya gavana ambaye inasemekana mshahara wake ni 4000£= 10Million za  Ki Tanzania kununua nyumba moja kwa gharama ya 2.2 million pounds sawa ma takribani Billion 2 na nusu za kitanzania, pia alinunua nyumba nyingine kwa  £ 311,000 (UK), pia kanunua mansion South Africa kwa £3.2Million, Magari kadhaa aina ya Range Rovers kwa £600,000, Gari aina ya Bentley £120,000, Mercedes Maybach kwa Euro 407,000.


Kweli Africa raha huyu ni kiongozi mmoja tu!! Je serikali zetu zina pesa kiasi gani? (TAFAKARI......!!!!!)


Kwa habari zaidi soma HAPA

10 April, 2012

KUMBE POLISI NAO HUIBIWA!!!

Habari toka majuu (Kwa Malikia/UK aka Ukerewe) zinasema maelfu ya pauni za Uingereza aka Great Britain Pound (GBP) yaliyokua mikononi mwa polisi yaibiwa. Pesa hizo ni zile ambazo zilikamatwa kutokana na upatikanaji wake kuhusisha njia ya udanganyifu na kuhifadhiwa katika ghala yenye ulinzi mkali katika kituo kimoja cha polisi wakati uchunguzi zaidi ukiendelea. Watu watatu walitiwa hatiani kuhusishwa na sakata hilo.Hata hivyo pesa hizo kiasi cha 113,000£ zapotea katika mazingira ya kutatanisha.Uchunguzi unaendelea na hakuna polisi wala raia aliyetiwa hatiani kutokana na upotevu huo..Inashangaza eti pesa ikaibiwa kituo cha polisi!!.Hivi polisi hazina bank accounts?.Kweli Duniani kuna mambo!!

Kwa habari zaidi soma HAPA

MAZISHI YA KANUMBA KUFANYIKA LEO KINONDONI MAKABURINI BAADA YA MISA NA KUAGWA RASMI VIWANJA VYA LEADERS CLUB




RATIBA YA MAZISHI YA MAREHEMU STEVEN KANUMBA

Kamati ya mazishi ya msanii Steven Charles Kanumba yatoa taarifa ya ratiba kwa vyombo vya habari ya utaratibu wa kumpeleka katika nyumba ya milele msanii huyo ambaye alikufa Ijumaa Aprili saba usiku.

Msanii huyo ambaye atazikwa katika makaburi ya Kinondoni amefanyiwa utaratibu ambao utamwezesha kila mwenye kuhitaji kushiriki mazishi hayo kuweza kumuaga. 

   Mwili wa marehemu utachukuliwa kwa msafara kutoka hospitali ya Taifa Muhimbili saa 2.30 asubuhi. Utapitishwa barabara ya Umoja wa Mataifa na Ali Hassan Mwinyi hadi viwanja vya Leaders Club, Kinondoni ambako Misa ya kumuombea itasomwa pamoja na salamu mbalimbali kabla ya watu wote kumuaga. 

Kamati hiyo imetoa wito kwa watu kujitokeza kwa wingi kuanzia saa mbili asubuhi kumuaga katika barabara ambazo atapitishwa . Saa 3.30 asubuhi mwili wa Kanumba utapokelewa viwanja vya Leaders ukitanguliwa na mapokezi ya wazazi wake, viongozi mbalimbali wa serikali ambao juu yao kabisa atakuwa makamu wa Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Dk Mohamed Gharib Bilal. 

 Saa 4.00 itakuwa ni muda wa kusoma Misa ambayo inakadiriwa kuchukua dakika 60 na saa 5 itakuwa kipindi cha salamu kutoka kwa watu mbalimbali. Saa 6.00 mchana ratriba ya kumuaga Kanumba itaanza mpaka saa 9.00 alasiri na baada ya hapo utakuwa wakati wa kuusafirisha mwili kwa msafara kutoka Leaders Club mpaka makaburi ya Kinondoni.Msafara huo utapitia barabara ya Tunisia, utakatisha barabara ya Kinondoni kuelekea makaburini. 

Sa 10.00 maziko yatafanyika kwa kufuata taratibu za imani ya marehemu. Kamati hiyo ya mazishi inayoongozwa na Gabriel Mtitu imewaomba wananchi watakohudhuria shughuli hiyo kwenda na maua ili kumuaga kwa heshima. Ibada na maziko vitafanyika kadri ya imani ya marehemu. Utulivu, unyenyekevu na ustahimilivu ni mambo muhimu yanayohitajika katika kipindi chote cha kumuaga mpendwa wetu Kanumba. 

BWANA ALITOA, BWANA AMETWAA. Sisi wote tulimpenda kwa dhati na tulitamani aendelee kuwa nasi siku zote ila Mungu aliyemleta kwa mapenzi yake ameamua kumchukua. Jina lake lihimidiwe. 

                     K.N.Y GABRIEL MTITU MWENYEKITI WA KAMATI YA MAZISHI


24 March, 2012

LCD TV ORIGINAL KWA BEI POA


Brand new Original Panasonic plasma Tv 50 Inch (127cm) for sale ***Made in the United Kingdom (UK)*** For Serious inquiry please email: rijaki@ymail.com OR Call: 0655 222523;Location: Dar es salaam.Delivery + Installation  free of charge (In Dar es salaam only)


NB:Other brands include Toshiba & LG , size from 40 to 50 inches.(  Zote ni flat screen  unaweza bandika ukutani,  pia utaletewa TV popote Dar na kuunganishiwa  bure)
 

Product Features and Technical Details
Product Features

• VIERA HD Ready 50-inch Plasma TV
• 100Hz Double Scan for ultra-smooth picture quality
• Dynamic Contrast 2,000,000:1
• VSmart Networking with VIERA Link and VIERA Image Viewer (integrating Photo and Video)
• Game Mode, V-Audio Surround

TV Tuner:
Integrated Tuners: PAL-I, DVB-T
Tele text Reception: 1000P Level 2.5, FASTEXT/LIST

Display
Screen Size: 50" (127 cm) diagonal
Panel: G13 Progressive HD Plasma Display Panel with Tough Panel
Viewing Angle: Viewing Angle Free
Resolution: 1,024 x 768 (16:9)
Applicable Scanning Format:
FULL-HD 1125: (1080)/50i, 1125 (1080)/60i, 1125 (1080)/24p (HDMI only), 1125 (1080)/50p (HDMI only), 1125 (1080)/60p (HDMI only)
HD: 750 (720)/50p, 750 (720)/60p
SD: 525 (480)/60i, 525 (480)/60p, 625 (576)/50i, 625 (576)/50p
Contrast Ratio (in dark surroundings): 2,000,000:1 Dynamic
Moving Picture Resolution: 720 lines
Intelligent Frame Creation: 100 Hz Double Scan
24p Smooth Film/Plaback Plus/Playback: 24p Playback
Shades of Gradation: 4,096 equivalent steps of gradation
Deep Colour (10/12-bit): yes
3D Colour Management: yes
Picture Mode: Dynamic/Normal/Cinema/True Cinema/Game/Photo
Vreal: Vreal 5

Sound
Speakers: 2 x 10 watt 2 Speakers
Sound Mode: Music/Speech/User
Virtual Surround: V-Audio Surround
Dolby Digital Out/CoNEQ: Dolby Digital

Input/Output
CI (Common Interface)*: yes
VIERA Image Viewer: yes (AVCHD/SD-VIDEO/JPEG playback)
HDMI Input/ Support Feature: 3 (1 side, 2 rear)/ Audio Return Channel (Input 2)
Composite Video Input: AV3: RCA phono type x 1 (side)
Audio Input (for Video): AV3: RCA phono type connectors (L, R) (1 set, side)
Component Video Input: RCA phono type x 3 [Y , PB, PR] (rear)
Audio Input (for HDMI, PC, Component) RCA phono type connectors (L, R) (1 set, rear)
21-Pin Input/output: AV1: AV In/Out, RGB In, Q-Link (rear) / AV2: AV In/Out, S-Video In, RGB In, Q-Link (rear)
Analogue Audio Out: RCA phono type connectors (L, R) (1 set rear)
Digital Audio Output (Optical): yes
Headphone Jack: 1 (side)
Features
EPG: yes
VIERA Tools: yes
VIERA Link: yes (HDAVI Control 5)
Multi Window: PAT
C.A.T.S. (Contrast Automatic Tracking System): yes
Game Mode: yes
Q-Link: yes
Off Timer: yes
Child Lock: yes

General
Wall mountable: yes
Power Save Mode: yes
Power Supply: AC 220 - 240 V, 50/60Hz
Rated Power Consumption: 265 W
On mode Average Power Consumption: 201 W
Standby Power Consumption: 0.4 W
Dimensions (W x H x D) (w/o stand): 1,218 x 769 x 93 mm
Dimensions (W x H x D) (with stand): 1,218 x 814 x 401 mm
Weight (w/o stand): 31.5 kg
Weight (with stand): 33.5 kg
Boxed product : 40kg
Wall Bracket: TY-WK4P1RW (not included)
Remote Control:Yes (included)

11 January, 2012

Laptops,Tv na simu bei poa.!!!!!!!

Kwa mahitaji ya laptops i.e Acer (i3 Processor,HDD 750GB,6GB RAM) ,Dell (INSPIRON 5030, HDD 500GB, 3GB RAM;Compaq (CQ50, HDD 250, 3GB RAM), 


1.Acer:(Grey,15.6'HDD750GB,Ram 6GB,Cam)







2.Dell:(Black,15.6'HDD 500GB,Ram 3GB,Cam)

3.Compaq:(Colour Black,15.4'' HDD 250GB,Ram 3GB,Cam)




Plasma Tv (flat screen) i.e Toshiba,Sony,LG,Panasonic,Samsung (size from 32 inch to 50) :Simu i.e iphone4 (Capacity 8GB, Black),BlackBerry Curve (ile mpya) no 9360,& Bold no 9900 (ile mpya), Nokia C5, N8 zote toka Uingereza.Kununua piga simu :0655222523, bei poa

14 December, 2011

2012 SCHOLARSHIPS FOR TANZANIANS-COVENTRY UNIVERSITY


Tanzanian 50 years Independence scholarship 2012

In association with the Tanzanian High Commissioner for the UK and the Institute of Accountancy Arusha (IAA), Coventry University are delighted to offer a limited number of full tuition fee scholarships for Tanzanian nationals.
Successful applicants will be awarded a place to study on one of these six courses:

How to apply

Applications are invited from Tanzanian nationals who meet the following criteria:
  • Applicants must be in possession of a degree from a recognised university with a first class or second upper (2:1) award
  • Applicants must provide evidence that they have made contributions to Tanzanian society in a voluntary or other capacity, or contributions that reflect Tanzania in a positive manner
  • Applicants applying for study in the UK must only apply if they have financial resources either personal or through a recognised sponsor to pay for their return flight, visa application and living expenses for the 12 month duration of the course.
To apply for the scholarship, complete the application form (Internet Explorer users should right click on the document and save the file to ensure compatability)

Email your completed application and supporting documents to Tnz2012scholarship@coventry.ac.uk
Closing date for applications 30 June 2012
The award decision will be made by Coventry University and will be based on the evidence provided within the application form.
For more info: CLICK HERE

11 November, 2011

HABARI NJEMA KWA BLOGGERS NAMNA YA KUBORESHA BLOG YAKO

UKIFUNGUA DASHBOARD KWENYE BLOG YAKO KAMA UNATAKA KUWEKA POST UTAONA KITU KAMA HIKI ''Learn more about Blogger's new look'' AU BONYEZA HAPA NA UFATE MAELEKEZO KUBORESHA BLOG YAKO NA ITAONEKANA KAMA HAPO CHINI.HAPPY BLOGGING!!

Using our upgraded interface

Along with several other Google products, Blogger’s taken on a whole new look: A clean, sleek interface designed for a streamlined blogging experience. Not only does the new interface load faster, but we’ve also added shortcuts to your most important blogging actions. Check out our quick list of what’s changed below.

Dashboard

Dashboard
Your Dashboard, as always, is your starting point. This is where all your blogs are listed, and you can click on the icons next to them to perform various actions on each blog, such as:
  • Writing a new post: Just click on the orange Pencil icon on your Dashboard to access the Post Editor.
  • Viewing your posts: The gray Post List icon will take you to a list of your published and drafted posts for a specific blog.
  • Catching up on your favorite blogs: Below the list of your own blogs, you’ll see a list of the blogs you follow with an excerpt from their latest posts.
  • Everything else: Check out the drop-down menu next to the Post List icon for a quick link to:
    • Overview
    • Posts
    • Pages
    • Comments
    • Stats
    • Earnings
    • Layout
    • Template
    • Settings
Note that the Earnings tab will only show if AdSense supports your language.

Overview

Overview
On the Overview tab, you can see your blog’s activity, news and tips from the Blogger team, and recent Blogs of Note.

New post


New post
To write a new post, just click on the orange Pencil icon from your Dashboard, next to the blog you want to post on. You’ll find the PublishSavePreview, and Close options at the top, and post options such as Labels and Schedules along the side.

New page


New page
Once on the Pages tab, you can click on the New Page button to choose whether you want readers to be directed to a new page that you create, or to another Web address.

Earnings


Earnings
Our Earnings tab is the new name for what used to be called Monetize. It’s just as easy to use, and we’ve got simple instructions to guide you through it.

Customizing your template


Template"
On the Template tab, you can either click on the orange Customize button to get started with our easy-to-use WYSIWYG (“What you see is what you get”) template designer, or choose one of our many default templates. If you’d like to edit the HTML of your blog, just click the gray Edit HTML button.

Permissions and Privacy

Permissions and Privacy

KAZI NYINGINE BANA MMHHH!!!


10 November, 2011

TANGAZO: WANACHAMA ZANZIBARWEBSITE MNAOMBWA KUZINGATIA.


Nachukua fursa hii kukusalimuni nyote wanaukumbi.
Hapa,Zanzibarwebsite ni pahala panapowaunganisha wazungumzaji Kiswahili popote walipo duniani.
Hilo ndio lengo mama.
Mengine kwa kupitia lugha yetu hii unapata haya yafuatayo:
  1. Kujifunza taaluma mbali mbali kupitia kwa wenzako waliokuzidi.
  2. Kujipatia taarifa mpya na zilizopita
  3. Kujipatia Rafiki /Shoga
  4. Kukutanisha na wenzako ambao mlipoteana kwa masiku.
  5. Kujiliwaza kwa picha/habari/mazungumzo/muziki n.k
  6. Kutumia uhuru wako wa kusema ( freedom speech) na kusikilizwa.
Hili la 6 - Ndio la kuwa makini - UHURU WAKO isiwe ukajisahau kutoheshimu UHURU WA WENGINE.
Ili kulinda mipaka ya uhuru wa wengine na wako mwenyewe ilipaswa haya yafuatayo uzingatie:
  1. Heshima na Nidhamu- usiropoke matusi makavu makavu.
  2. Usilete mas-hara ya kuchupa mipaka ya kumuingia mtu maungoni - kiasi cha mtu kujiona amedhalilishwa ama kudharauliwa.
  3. Epukana na Ubaguzi wa aina yeyote iwe rangi/jinsia/kabila au wakimajimbo.
  4. Uwe tayari kutoa mchango ili na wewe uchangiwe  mawazo.
  5. Uwe tayari kukosolewa pale unapokosea.
HAYA YAKIZINGATIWA NA KUFANYIWA KAZI - Zanzibarwebsite will be the place of leisure,educative,harmony and more communicative one rather than others.
Shime wadau- HESHIMA NI KITU CHA BURE
Babengwa wa Upendo.
Zaidi watembelee  Zanzibarwebsite

Last day to vote for Tanzania's Mt.Kilimanjaro as one of the 7 Natural Wonders of the World


If you have not already voted for Mount Kilimanjaro, what are you waiting for?  Only 7 countries will become home to one of the 7 Natural Wonders of the World, and only these 7 countries will reap the rewards of this distinction.  Voting closes this Friday at 2 PM.
Below are 10 great reasons why you should vote for Mt. Kilimanjaro today.  Please take 5 minutes and cast your vote now.  You can also help to spread the word by posting this on your blog, Facebook page and emailing it to everyone you know that cares about Tanzania.
To cast your vote now, please visit http://www.new7wonders.com/vote-2
 
Vote for Kili Flier

20 October, 2011

CHANGAMOTO YA LEO

KUTOKANA NA MATATIZO YA FOLENI ZA HAPA NA PALE JIJINI DAR ES SALAAM PIKIPIKI (MAARUFU KAMA BODA BODA) IMEKUA KAMA MKOMBOZI JAPO KUNA TATIZO.HIVI HAWA WAENDESHAJI PIKIPIKI LESENI WANAPATA ZA HALALI? KAMA NI HALALI KWANINI AJALI NI NYINGI? NADHANI KUNA HAJA YA WATU WANAOFANYA BIASHARA HII KUA NA MAFUNZO MAALUMU YA LAZIMA KULINDA MAISHA YAO PAMOJA NA ABIRIA AMBAO WANAWABEBA.ALIYETENGENEZA HII PICHA HAJAKOSEA NI KWELI SASAHIVI KUA/KUPANDA PIKI PIKI NI SAWA NA KUTAFUTA  ULEMAVU TENA WA KIZEMBE KABISA.WAJIBU WA SERIKALI HAPA NI KUTOA LESENI HALALI NA KUZIKAGUA MARA KWA MARA, PIA MTUMIAJI WA CHOMBO KAMA HIKI THAMINI MAISHA YAKO KWANINI UENDESHWE NA  MTU ALIYELEWA,HANA UZOEFU AU ANAPITA SEHEMU YA HATARI NAWEWE UNAMUANGALIA TU? SERIKALI HAIWEZI FANYA KILA KITU KUA MWANGALIFU!!

(KAMA PICHA YAKO TUWASILIANE SIKUMBUKI NIMEITOA WAPI NINGEKUSHUKURU)

TATIZO LA AJIRA LIPO KILA SEHEMU

                            Watu 500 wapanga mstari kuomba kazi (nafasi 20 tu) UK

Kufuatia kuanguka kwa uchumi kuanzia mwaka 2008/2009 ambako kumeathiri mzunguko wa fedha nchi mbalimbali duniani ambapo kila serikali iliweza jitahidi kunusuru uchumi wake kwa namna yake.Hapa Uingereza Gordon Brown alilazimika kuuza nusu ya dhahabu ya nchi kunusuru uchumi ulio yumba.(soma hapa).USA nao wali inusuru nchi kwa $700 Billion (soma hapa).Anguko hilo la uchumi lilipelekea makampuni mengi kufungwa na kupoteza ajira za watu wengi sehemu mbalimbali duniani.Hapa UK watu zaidi ya 2 million hawana ajira hivi sasa na serikali ndio inawagaramia kwa job seekrs allowance (kwa wazawa na wenye sheria ya kuishi nchi hii)


Sijashangaa kuona msururu ulijitokeza Chuo kikuu Dodoma kwa nafasi 12 za ajira.Ila nimeshangazwa na utaratibu wa kuita watu zaidi  ya 2000 kwa nafasi 12 za ajira.
    Ati msururu wote huu waitwa kwa usaili wa nafasi 12 za kazi!!! hivi inaingia akilini??
   (picha kwa hisani ya Bongo Pix Blog)

Hii ni kuchezea akili za watu huwezi ita (shortlist) watu 2000 kwa nafasi 12.Hawa watu wanasafiri toka sehemu mbalimbali sio ustarabu kuita watu wote hao kwa nafasi hizo chache (soma hapa na hapa).Hii ni sawa na shule/chuo kinachochukua wanafunzi 100 kutoa fomu laki moja za kuomba nafasi tena kwa kulipisha watu pesa huu ni wizi wa hali ya juu sana.Ufisadi sio lazima mtu ale rushwa hata huu ni ufisadi.

14 October, 2011

LEO NI SIKU NA MWEZI AMBAO BABA WATAIFA ALIIAGA DUNIA


Julius Kambarage Nyerere (13 April 1922 – 14 October 1999)

LEO TAREHE 14 MWEZI WA 10 NI SIKU NA TAREHE AMBAYO TUNA ADHIMISHA KUMBUKUMBU YA KIFO CHA BABA WA TAIFA MWALIMU JULIUS KAMBARAGE NYERERE NA RAIS WA KWANZA WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA.SIKU HII NI SIKU MUHIMU KITAIFA NA PENGINE KIMATAIFA KATIKA HISTORIA YA TANZANIA NA AFRICA KWA UJUMLA.KATIKA KUMBUKUMBU HII NI VEMA SERIKALI NA WATANZANIA KWA UJUMLA KUKUMBUKA MAMBO MUHIMU AMBAYO MWALIMU ALIKEMEA KW ANGUVU ZAKE ZOTE.MFANO WA MAMBO HAYO NI RUSHWA (CORRUPTION) MAARUFU KAMA KITU KIDOGO.

RUSHWA IMEKUA KAMA  MCHEZO AMBAO UMEZAGAA TANZANIA NA AFRIKA KWA UJUMLA.SASA HIVI HATA UKITAKA HUDUMA YA AFYA YA HARAKA NI LAZIMA UTOE KITU KIDOGO.HUDUMA YA BURE BILA KITU KIDOGO HUWEZI PATA KWA MUDA UNAOTAKIWA.MCHEZO HUU MCHAFU UMEKUA KWA KIASI KIKUBWA KIASI KWAMBA KUNA WATANZANIA WANA AMINI BILA RUSHWA HUWEZI FANYA LOLOTE.

MADHARA YA RUSHWA NI PAMOJA NA KUTO KUWAJIBIKA KWA VIONGOZI WETU,UONGOZI USIO WA SHERIA,MAADILI WALA HAKI,AJALI,VIFO,MAENDELEO DUNI,HUDUMA MBOVU KWA JAMII MFANO HUDUMA ZA AFYA,ELIMU,BARABARA  N.K.ITAMBULIKE WAZI KATIKA MAADHIMISHO YA KUMBUKUMBU YA MWALIMU KUA RUSHWA BADO NI ADUI MKUBWA ALIYEKOMAA NA KUIDIDIMIZA TANZANIA KATIKA NYANJA ZA KIUCHUMI,KIJAMII,KISIASA NA KIUTAMADUNI.TAASISI YA KUPAMBANA NA KUZUIA RUSHWA (TAKUKURU) IWE CHOMBO HURU NA CHENYE NGUVU KUWAJIBISHA WATUHUMIWA WA RUSHWA WANAPO BAINIKA BILA KUJALI NANI,CHEO,DINI WALA KABILA.ITAKUA HAINA MAANA KILA SIKU TUWE TUNASIKIA TAKUKURU WAMKAMATA  KAMANDA FEKI HUKO SIJUI WAPI!


MANENO HAYA YA MWALIMU YAPO AU HAYAPO? KAMA YAPO MBONA HATUONI WALIO KULA FIMBO 12 NA KUWAONYESHA WAKE ZAO WAKIWA WANATOKA JELA?.RUSHWA NI ADUI MKUBWA WA HAKI!


SOMA ZAIDI HAPA KUHUSU HISTORIA YA MWAL.NYERERE

Umar Farouk Abdulmutallab to face life sentence!!

                                                              Umar
 Umar Farouk Abdulmutallab pleaded guilty to trying to blow up a transatlantic flight on Christmas Day 2009.Having pleaded guilty at his trial in Detroit, he is set to face life in prison when he is sentenced on 12 January 2012.Umar is a Nigerian born man aged 24 year old,privileged,very religious and teacher's dream.According to Michael Rimmer, a Briton who taught him history, told the BBC Umar Farouk Abdulmutallab had been "every teacher's dream - very keen, enthusiastic, very bright, very polite".[BBC]


Abdulmutallab's father, Alhaji Umaru Mutallab, said he had approached the US and Nigerian authorities to warn them about his son's views in November - weeks before the attempt to destroy the flight to Detroit with at least 300 passengers on board.


FIKIRIA HUYU NI MTOTO WAKO!!..HIVI KAMA MZAZI UNAPOONA MTOTO ANAENDA KUSIKO UNAKAA KUMUANGALIA AU UNACHUKUA HATUA? JE MZAZI WA UMAR ANAJISIKIAJE KUMKOSA MTOTO WAKE KWA MAISHA YAKE YOTE? JE ANGEMUONYA AMA KUMLAZIMISHA KUBADILI MISIMAMO YAKE SI ANGELISAIDIA KUOKOA MTOTO WAKE? KIJANA MDOGO KAMA HUYU SASA ATATUMIKIA KIFUNGO CHA MAISHA KWA FAIDA YA NANI? JE KUNA WAZAZI WANGAPI WA NAMNA HII? MTAZAMO WANGU MZAZI WA UMAR AMESHINDWA KUWAJIBIKA KIASI FULANI KAMA AKWELI ALIONA MTOTO WAKE ANAPOTEA ANGEFANYA KITU KUMUOKOA. JE UNGEKUWA WEWE MZAZI WA UMAR UNGEFANYAJE UNAPOONA MTOTO WAKO ANAPOTEA? KUTOA TAARIFA VYOMBO VYA DOLA BILA KUFANYA JITIHADA ZAKO KAMA MZAZI HAITOSHI NA HAIKUSTAHILI MTAZAMO WANGU. JE WEWE UNASEMAJE?


ZAIDI SOMA HAPA NA HAPA

MONEY vs HUMANITY


Nionavyo mimi pesa na utu wa mtu ni vitu viwili muhimu katika maisha ya kila siku, bahati mbaya siku zinavyo zidi kwenda uwepo wa pesa umekua na maana zaidi kuliko utu wa mtu.Kwanini? Mtu anaweza muondoa uhai mwenzie kisa anataka kupata pesa..Mtu yupo tayari kutafuta pesa hata kwa gharama ya maisha ya mtu mwingine.Sasa hivi imekua kawaida mtu ukisema kitu kama huna pesa basi husikilizwi kama umeongea cha maana.Aidha ukiwa na pesa unaweza fanya chochote kihalali au kinyume chake bila wasiwasi kwani pesa itakulinda.Hii ni sifa kubwa katika nchi zinazo endelea japo hata zilizo endelea kuna nafasi ya pesa lakini utu wa mtu una maana zaidi na hivyo pesa haiwezi kukulinda unapo hatarisha utu wa mtu kwa kutumia pesa zako.Je nchi yetu Tanzania inaona hili?


Ukitaka kuona kama pesa inamaana zaidi angalia picha hapo juu, sasahivi kuna maelfu ya watu Somalia na nchi jirani wakiwa na janga la njaa, maisha ya watu wengi yapo hatarini na muamko wa watu kutangaza janga hilo ni mdogo sana kulinganisha alipo kufa mwanzilishi wa kampuni ya Apple ambapo kila mtu ameonyesha kuguswa naye kwa namna moja ama nyingine.Je ni kwasababu alikua na pesa?, alitoa ajira nyingi? katoa bidhaa inayopendwa? mbunifu wa kihistoria katika maendeleo ya teknolijia?.jibu linaweza kua ni ndio lakini kwanini watu hawaguswi na hawa watu wanaokufa kila siku kwa kukosa chakula? ajali za kizembe kama zile za kuzidisha mizigo kwenye vyombo vya usafiri kwa manufaa ya watu fulani?.Je ni lini utu wa mtu utathaminika?

Things are back to normal on BlackBerry

This  made a headline  on various media after many of its users in Europe, the Middle East and Africa lost services on Monday.The BB users suffered problems with email, BBM and internet that were reported by customers later that day.Canadian firm Research in Motion (RIM) has apologised for the inconvenience and says that all services have now been restored.
Apparently there's no official word yet from RIM on what caused the problem but it's reported to be linked to a crashed server at a BlackBerry data centre.This  indeed will be another huge blow to the company and its reputation apart from the weaker sales in the face of strong competition from Android handsets and Apple's iPhone.

12 October, 2011

BLACKBERRY BLACKOUT ENTERS 3RD DAY



A global BlackBerry outage has entered its third day with users more fed up than ever with the disruption to their e-mails, instant messaging and Internet.

The BlackBerry outage, which began at 11am BST on Monday, left 10 million smartphone owners across Europe, the Middle East and South America with limited access to data services.

In an update from the BlackBerry maker last night, Canadian company Research in Motion(RIM) explained the glitch. “The messaging and browsing delays being experienced by BlackBerry users in Europe, the Middle East, Africa, India, Brazil, Chile and Argentina were caused by a core switch failure within RIM’s infrastructure.

TUKO WAWILI PEKEE YETU!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!


Ni kweli Mungu anasamehe lakini unapomueleza binadamu mwenzio ubaya huu
unategemea nini................????????????
Padri amekaa katika ki-box cha kuungamisha, kanisani hakuna mtu. Mara muumini mmoja akaingia, akapiga magoti upande wa pili na kufanya ishara ya msalaba akaanza kuungama.
"padri naungama dhambi zangu, leo nimefanya dhambi kubwa sana "
"endelea"
... "bosi wangu aliniita nyumbani kwake akaniambia amegundua nimeiba shilingi milioni 50, akasema nisipotoa maelezo ya kutosha atanipeleka polisi. Sasa ukweli mimi naogopa kufungwa, nikatazama huku na huku nikagundua tuko wawili peke yetu, nikachomoa bastola nikamuua. Yesu atanisamehe?
"utasamehewa"
"Basi wakati nataka kuondoka nikasikia mlango unafunguliwa, kutazama loh, mke wa bosi. Akaniuliza nimemfanya nini mume wake. Kutazama huku na huku nikagundua tuko wawili peke yetu, nikamuua na yeye. Yesu atanisamehe na hiyo?"
"utasamehewa"
"nikatoka nje, nikawasha gari niondoke lakini mlinzi akakataa kufungua geti akasema amesikia kama kishindo hivi! Nikaona ananiwekea kiwingu. Kutazama huku na huku nikagundua tuko wawili peke yetu nikamuua. Yesu atanisamehe?"
"utasamehewa"
"nikajifungulia geti mwenyewe nikaenda nyumbani, wakati napanga kuja kuungama mtoto wa bosi akabisha hodi nikawaza mambo gani tena. Akasema amerudi nyumbani na kukuta yaloyotokea, lakini akanionyesha diary ya baba yake inayoonesha kuwa nilikuwa na appointment naye kabla hajafa. Nikamuuliza nani mwingine anajua, akasema ameanzia kwangu kisha atakwenda polisi. Nikatazama huku na huku nikagundua tuko wawili peke yetu nikamuua. Diary nikaichoma moto. Yesu atanisamehe na hilo ?"
- kimya........
"padri, Yesu atanisamehe kwa hilo ?"
- kimya.........
Jamaa kutazama kwenye kibox padri hayupo. Lakini kwenye kona moja akaona kabati la ngou za mapadri kama linatikisika. Kufungua akamuona padri kajificha katikati ya majoho anatetemeka.
"sasa baba mbona umenikimbia?"
padri kwa taabu akajibu "nilitazama huku na huku nikagundua kuwa tuko wawili tu peke yetu........"

                 ''AISEE ULIYE ANDIKA HII HONGERA KWA UBUNIFU''