16 August, 2011

TUNES OF THE WEEK (BONGO FLAVA)

Hii leo ndio list yangu ya Miziki mizuri ya Tanzania (Bongo flava) ikiongozwa na AY ft Lil Romeo,Lamyia.Hizi ni baadhi ya nyimbo bora za wasanii wetu siunajua mcheza kwao hutuzwa basi unaweza sikiliza kwa kubonyeza moja baada ya nyingine .Raha jipe mwenyewe usisubiri kupewa.




HIVI KWELI MAPENZI SUMU?

Kwa wale ambao wamekwisha chukua maamuzi magumu ya kuoa hasa miaka yasasa wanaweza kua na majibu  sahihi ya hili swali.Lakini pia katika harusi zote nilizo hudhuria hua sikosi kusikia ''MKAVUMILIANE NA KUHESHIMIANA'' hivi vitu viwili vikikosekana lazima ndoa iyumbe kwa namna moja ama nyingine.Hata hivyo ndoa sasa hivi hazidumu je tukubali kua mapenzi ni sumu?.Kimtazamo kama usemi huu una ukweli  kwa asilimia kubwa basi ishakua balaa!!

Mie nilikua nadhani ukiwa na mpenzi (Mke/Mme) basi ni raha kumbe inaweza kua kinyume chake.Na kwakua sasahivi ndio wanaita muda wa haki sawa,kwenda na wakati basi talaka ndio nje nje tujiulize kwanini?.Mbali na hio vijana sasahivi wanachelewa kuoa/kuolewa je tatizo ni nini?? Wengine wanasema ndoa ndoano je hii ni sababu ya ambao hawajaoa kutooa mapema?

Mtazamo wangu, kwakua imekua mila na desturi sehemu nyingi Africa hususani Tanzania toka zamani tumeona mwanaume ndio mtoa maumuzi ya mwisho (aka kichwa cha familia) si vibaya kwasasa mwanamke kushirikishwa katika maumuzi mbalimbali katika familia.Kusingizia haki sawa miongoni mwa wanawake na kujenga kiburi mwisho wake talaka.


Ni lazima kuheshimiana na kusikilizana kwa wapenzi/wanandoa (kama mnataka kufurahia).Mambo uliyofanya ukiwa pekee yako lazima uangalie kama yana mchango mzuri katika mahusiano kama sivyo basi achana nayo.Imekua utaratibu sasa hivi wapenzi kusema wanataka uhuru unakuta mtu kaoa/kaolewa na bado ana mawasiliano ya karibu na mpenzi wa zamani ya nini hasa?


 Hii tabia sio nzuri ndo mwanzo wa kupokelea simu chooni,kuzima simu ukiwa na wako,kuweka silent na kuwekeana password ambazo huongeza maswali ni je unaficha nini?? Mambo ya vidumu mpaka lini na magonjwa yaliyozagaa?? Nadhani hii ni moja ya sumu ya mapenzi, na kwanini tusiite mapenzi raha/matamu na maneno kama hayo kwa kuepuka hizo sumu ambazo ziko wazi?

MUWEKEZAJI AKIONA MANENO HAYA LAZIMA AKIMBIE SANA.


Au wewe unaonaje? Hii kwa muwekezaji haina maana tofauti na ile ya mzazi (anaye penda mtoto afauru) kupeleka mtoto wake shule ambayo anaambiwa haina walimu,vifaa vya kufundishia,mtoto atakaa chini (hakuna viti vya kutosha) wakati anasoma,hakuna vitabu,maktaba n.k huyu atakua mzazi wa ajabu katika dunia hii.Sasa tujiulize ni muwekezaji  gani toka ndani/nje atatamani kuwekeza nchi haina umeme,maji na mafuta??.
Kipengele cha hakuna serikali (No Government) siamini labda tuseme haijawajibika katika baadhi ya mambo.