09 August, 2011

VURUGU ZA LONDON ZASAMBAA MIJI MINGINE

Kumezuka vurugu jijini London Uingereza baada ya raia mmoja kupigwa risasi na polisi.Vurugu hizo zilizuka baada ya polisi kuzuia maandamano ya amani na kuhoji kwanini raia Mark Duggan (29) aliuawa na polisi kwa kupigwa risasi? Tukio hilo lilitokea Tottenham Alhamis Tar 04 na Jumamosi ya tarehe 06/08/2011 ndipo vurugu zilipozuka eneo hilo na kusambaa miji kadhaa hapa England.
Mark Duggan,29 wakati wa uhai wake


Hali hiyo ya vurugu imeingia kwa kasi miji mingine kama Birmingham,Liverpool,Manchester na Bristol.Ukiachia mbali huyu jamaa kuwa chanzo maisha magumu,ukosefu wa ajira unaozidi kukua na ubaguzi wa rangi vimetajwa kuchangia vurugu kuungwa mkono kwa kasi.Waziri mkuu David  Cameron aliyekua mapumzikoni Italy amelazimika kurudi kwani hali ni tete.Jana 08/08/2011 Birmingham palikua hapatoshi.

 Jengo limechomwa moto Croydon
 Polisi ambao walizidiwa nguvu wakiwa wanaangalia kinacho endelea kama kideo!
 maduka,magari yalichomwa moto
 Mtaani kulikua kama hivi
Jamaa  wenye mask wakiiba dukani na kuvunja ATM machine na kuiba Pound!
Picha zote toka Aljazeera na BBC
Kwa habari zaidi soma HAPA na HAPA

WANAWAKE WADAIWA KUBAKA WANAUME!!!

Huko kwa Mugabe nchini zimbabwe kuna tuhuma za wanawake kuwabaka wanaume kwa makusudi .Ubakaji huo umedaiwa kukua siku hadi siku kwani kwasasa ni kila wiki lazima mwanaume abakwe!.Mkuu wa polisi jijini  Harare Angeline Guvamombe amesema “  wanawake wanao endesha magari ya kifahari huwapa wanaume lifti na kuwapulizia maji maji usoni yanayowafanya wasinzie na baadae kulazimisha kufanya nao mapenzi'' Kwa mujibu wa  the Herald  wiki mbili zilizo pita wanaume wawili walitekwa na kulazimishwa kufanya nao mapenzi chini ya usimamizi wa bunduki. Wakati katika tukio lingine wanawake watatu walimteka mwanaume wa miaka 30 na kumlazimisha kufanya nae mapenzi kwa siku 5!!.


Cha ajabu tangu ubakaji huo kuanza hakuna mtu amekamatwa kwa kosa hilo na polisi wamesema wanawake hawawezi shitakiwa kubaka kwani sheria ya Zimbabwe haitambui kama mwanamke anaweza mbaka mwanaume na hivyo mwanamke anayebaka anaweza shitakiwa tu kwa kumvamia mwanaume kwa nguvu (assault) na kupata adhabu ndogo ikilinganishwa na ile ya mwanaume kubaka.


Hii ni changamoto katika nyanja ya sheria kwani mabadiriko ya wakati yamebadirisha mfumo wa mahitaji.Je kwetu Tanzania hali ikoje katika maswala haya? Wanasheria tuambieni ili tujue mie nikibakwa nijue kama haki yangu ipo ama laa kwani kwa mpango huu hakika wanaume watakua hatarini kuambukizwa magonjwa ya zinaa bila kupenda!



Kwa habari zaidi soma: HAPA