Showing posts with label Tanzania.. Show all posts
Showing posts with label Tanzania.. Show all posts

21 May, 2013

JE WATAKA KUSOMA UINGEREZA-COVENTRY UNIVERSITY WALETA MWAKILISHI TANZANIA.


Kwa wale ndugu jamaa na marafiki ambao mngependa kusoma chuo Uingereza (UK) hasa Coventry University mnaweza soma maelezo hayo hapo chini.Nimeona si vibaya na nyie mkapata fursa ya kuonana na mwakilishi toka  Coventry kwa maelezo zaidi.Hii barua pepe nilitumiwa mimi (Rik) kwani ni mhitimu wao na mimi sio mchoyo nawapa kama ilivyo, endele kupata maelezo chini
                      LIBRARY

Habari,

I will be in Dar es Salaam, Tanzania on 19th – 25th May 2013 in my official capacity as Coventry University, East & Southern Africa Operations Manager, to meet students who have applied to study at Coventry and anyone who may be interested in applying to the University, enquiring about the courses available, entry requirements, visa process and any other official enquiry

For FREE registration or consultation, you are welcome to come meet me at my hotel on appointment from 19th – 25th May 2013:

Hotel
Harbourview Suites,
Harbourview Towers,
Samora Avenue,
Dar es Salaam - Tanzania.

For appointment
Call: +254 716 062 100

You can also meet me at the Tanzania Commission for Universities, 8th Exhibition on Higher Education, Science and Technology.
LOCATION: - Dar es Salaam, Tanzania
VENUE: - Diamond Jubilee Hall
DATE: - 22nd - 24th May
TIME: - 12pm - 6pm (Daily)

Please feel free to invite any friend or family that may be interested in applying to Coventry University

I look forward to seeing you soon.

Best wishes

Silpa


SILPA A. NYAGUDI,
East & Southern Africa Office, Operations Manager
Coventry University

MOBILE 1: +254 716 062 100
MOBILE 2: +254 723 161 908
SKYPE: silpa.kenya.coventry

“Ranked No.46 UK University*”

“Entrepreneurial University of the Year - Times Higher Education Awards 2011”


                                                         ADMINISTRATION BLOCK


Chuo cha Coventry nao wakanitumia hii hapa chini;

Meet Coventry University Staff

Dear Rikard
Silpa Nyagudi, Coventry University East and Southern Africa Operations Manager, will be in Tanzania to support students considering Coventry University as their future study destination. 
Event: Meet Coventry University Staff
Date: 19th - 25th May 2013
Venue: Harbourview Suites, Harbourview Towers, Samora Avenue, Dar es Salaam (hotel).
Event: Tanzania Commission for Universities, 8th Exhibition for Higher Education, Science & Technology
Venue: Diamond Jubilee Hall, Dar es Salaam, Tanzania
Date: 22nd - 24th May
Time: 12pm - 6pm
If you would like to meet with Silpa to discuss study opportunities available at Coventry Univeristy, Please make an appointment using the contact details below:
Call: +254 716062100 or +254 723161908
Email: aa7167@coventry.ac.uk



10 November, 2011

Last day to vote for Tanzania's Mt.Kilimanjaro as one of the 7 Natural Wonders of the World


If you have not already voted for Mount Kilimanjaro, what are you waiting for?  Only 7 countries will become home to one of the 7 Natural Wonders of the World, and only these 7 countries will reap the rewards of this distinction.  Voting closes this Friday at 2 PM.
Below are 10 great reasons why you should vote for Mt. Kilimanjaro today.  Please take 5 minutes and cast your vote now.  You can also help to spread the word by posting this on your blog, Facebook page and emailing it to everyone you know that cares about Tanzania.
To cast your vote now, please visit http://www.new7wonders.com/vote-2
 
Vote for Kili Flier

20 October, 2011

TATIZO LA AJIRA LIPO KILA SEHEMU

                            Watu 500 wapanga mstari kuomba kazi (nafasi 20 tu) UK

Kufuatia kuanguka kwa uchumi kuanzia mwaka 2008/2009 ambako kumeathiri mzunguko wa fedha nchi mbalimbali duniani ambapo kila serikali iliweza jitahidi kunusuru uchumi wake kwa namna yake.Hapa Uingereza Gordon Brown alilazimika kuuza nusu ya dhahabu ya nchi kunusuru uchumi ulio yumba.(soma hapa).USA nao wali inusuru nchi kwa $700 Billion (soma hapa).Anguko hilo la uchumi lilipelekea makampuni mengi kufungwa na kupoteza ajira za watu wengi sehemu mbalimbali duniani.Hapa UK watu zaidi ya 2 million hawana ajira hivi sasa na serikali ndio inawagaramia kwa job seekrs allowance (kwa wazawa na wenye sheria ya kuishi nchi hii)


Sijashangaa kuona msururu ulijitokeza Chuo kikuu Dodoma kwa nafasi 12 za ajira.Ila nimeshangazwa na utaratibu wa kuita watu zaidi  ya 2000 kwa nafasi 12 za ajira.
    Ati msururu wote huu waitwa kwa usaili wa nafasi 12 za kazi!!! hivi inaingia akilini??
   (picha kwa hisani ya Bongo Pix Blog)

Hii ni kuchezea akili za watu huwezi ita (shortlist) watu 2000 kwa nafasi 12.Hawa watu wanasafiri toka sehemu mbalimbali sio ustarabu kuita watu wote hao kwa nafasi hizo chache (soma hapa na hapa).Hii ni sawa na shule/chuo kinachochukua wanafunzi 100 kutoa fomu laki moja za kuomba nafasi tena kwa kulipisha watu pesa huu ni wizi wa hali ya juu sana.Ufisadi sio lazima mtu ale rushwa hata huu ni ufisadi.

21 July, 2011

RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO YA TANZANIA ATOA UFAFANUZI SWALA LA UMEME

KUSIKILIZA UFAFANUNUZI WA TATIZO LA UMEME TANZANIA KUTOKA KWA MHESHIMIWA RAIS MH JAKAYA MRISHO KIKWETE FATA LINK HAPO CHINI ALIVYO HOJIWA NA MWANDISHI WA BBC BWANA OMAR MUTASA.RAIS ANASISITIZA WATANZANIA MUWE NA SUBIRA SERIKALI INAFANYA JITAHADA KUBWA LAZIMA WATU WATAMBUE NA KAMA KUNA MTU ANA MAARIFA YA HARAKA KATIKA KUTOA UFUMBUZI WA UMEME BASI AYATOE SERIKALI ITAYAFANYIA KAZI.


ZAIDI SIKILIZA RAIS AKIFAFANUNUA KUHUSU UMEME KWA KUBONYEZA HAPA





08 June, 2011

MAISHA BORA KWA KILA....

Ndugu msomaji hapo chini ni picha ya usafiri wa Trekta huko Ludewa.Huu ni mfano tu wa maisha halisi watanzania walio wengi katika maeneo mbali mbali nchini Tanzania.Kwa anaye ishi mjini atashangaa kuona maisha kama haya ila huo ndio ukweli wenyewe huko vijijini.Hapo walipo sina hakika hata wamevaa chochote miguuni ukimuondoa dereva lakini  wao wanaona ni maisha ya kawaida na wameshazoea..

Je mimi na wewe nani angependa kuishi maisha haya?  Ni kweli serikali haiwezi fanya kila kitu kuboresha maisha ya kila mmoja lakini je  hawa watu wamewezeshwa kujikwamua na maisha magumu? hua tunaambiwa kuna pembejeo za ruzuku je zinawafikia walengwa kwa bei nafuu kama ilivyo pangwa?  Ok tumewapa pembejeo za ruzuku ambazo sina hakika kama ni 'ruzuku' hizo bara bara za kupitisha mazao japo kwenda kuuza zipo?? Na mwisho kabisa niseme tu kama mlikua hamjui hawa ndio wapiga kura wetu kwa asilimia kubwa, swali je maisha  bora kwa kila mtanzania yapo au ni kauli mbiu tu ya kisiasa? maana hata bara bara yenyewe hapo mie sijaona ni kama wanakatisha porini tu au macho yangu?.



                               Picha kwa hisani ya mzee wa matukio: Francis Godwin wa                http://francisgodwin.blogspot.com/. kwa habari na picha zaidi bofya hapo uone maisha bora kwa kila Mtanzania!!


Aidha sehemu kama hii nikiambiwa ambulance au gari ya kubebea wagonjwa ni kama hizi hapa sita shangaa
                                           Ambulance hii sijui ni ya wapi?




                                  Hii sijui niite nini.. ilimradi mgonjwa afike (na sina hakika kama atafika!!!)


 Hakika sitabisha kwasababu maisha haya nayajua na kuna sehemu ambazo nisha tembelea (vijijini) ukiumwa na ukapona mshukuru Mungu maana hata mie nili nusurika kufa huko hata kama una pesa hazitakusaidia maana hakufikiki kirahisi .Na sidhani kuna kiongozi mkubwa wa nchi ashawahi fika huko vijijini japo wana magari mazuri kama Land Cruiser VX/V8 na mengine ambayo wanatembelea mjini kwenye lami ambako hata Rav4 ingefaa!!.


Yaani hata wazungu watoa misaada nina imani hawaishi kushangaa wanavyoona usafiri wetu (viongozi) halafu unaita nchi masikini hapo hapo kuna mtu (Mtanzania) anapanda trekta  kusafiri tena ni mpiga kura (mwananchi)  wakati mpigiwa kura (kiongozi) anapanda  Land Cruiser V8 kwa jasho la mpanda trekta hivi hii ni haki kweli? Na kwanini apande trekta na sio bus? jibu la haraka hapo ni miundo mbinu mibovu hakuna mtu atathubutu kupeleka bus huko labda serikali yenyewe ifanye hivyo kama zamani yale ma bus ya serikali sijui yalifia wapi? Magari ya kusafirisha mizigo mfano Iringa kulikua na IRINGA RETCO,Mbeya MBEYA RETCO yale yalikwenda wapi?