04 August, 2011

Professor Jay - Kama Ipo (Video)


TUSIFIKIE TU HATUA HII .....ha ha haa !!!

Kufuatia sakata la kufukuzwa wabunge  toka mjengoni katuni hapa chini imenifurahisha sana kwa namna ujumbe ulivyofikishwa.Sasa tukifikia hatua kama hii sipati picha Bunge litakuwaje.Nadhani mchora katuni  ameonyesha  dawa ya uonevu ipo jikoni ipo siku utapatiwa suluhu ya namna hio ama inayoendana ili kwenda sawa ama kukomesha hali hio kabisa.Tujiunge ha ha haaaa!!! yani sina mbavu.Hongera Abdul




                                      Kesho kutwa!!!!?

Sasa hii ya hapa chini sijui wanamfurahisha nani? Kama bajeti haifai kwanini uipitishe? Huyu ndio mwakilishi wa mpiga kura!! Je tuseme wabunge wa namna hii hawajui majukumu yao bungeni?? Nadhani wabunge wa namna hii ndio wafukuzwe bungeni hawana faida na mwisho wataishia kulala tu wakati mjadala ukiendelea!
                          Kuna mwenye majibu swali ndio hilo, sema usikike!

HOSNI MUBARAK KUVUNA ALICHOPANDA!


Aliyekua Rais wa Misri (Egypt) Hosni Mubarak-83 ambaye alijiuzulu kufuatia maandamano makubwa kufuatia tuhuma za rushwa na uongozi wa mabavu.Mnamo April,2011 aliwekwa chini ya ulinzi bila kujali afya yake iliyozorota na jana (Jumatano Agasti 03,2011)  pamoja na hali yake kiafya kuyumba alifikishwa mahakamani kujibu mashtaka ya rushwa iliyo kithiri,kuua waandamanaji jitihada ambazo hazikuzaa matunda mpaka alipo achia ngazi mwezi Januari 2011. Wakati huo huo hali ya Misri bado tete kutokana mvurugano uliopo kati ya serikali ya sasa na waombolezaji ambao walizuiwa kuandamana ikiwa ni ishara ya kuwakumbuka watu waliopoteza maisha katika harakati za kumtoa Mubarak


Mubarak pamoja na mwanaye wamekana mashataka dhidi ya Rushwa na mauaji ya waandamanaji na kwa sasa waandamanaji wameahidi kutulia wakisubiri hukumu itolewe kwa Mubarak na vibaraka wake.Japo waliofika mahakamani waliweza wafukuza polisi kwa mawe. HII NI CHANGAMOTO KWA SERIKALI ZETU KATIKA UWAJIBIKAJI NA MATUMIZI YA NGUVU WANAPOWAKOSEA WANANCHI (WAPIGA KURA),KASHFA ZA RUSHWA NA UWAJIBISHWAJI.


Kwa habari zaidi soma HAPA,HAPA,HAPA na HAPA