31 March, 2011

MWAKA WA VIKOMBE NI HUU, MORO KUMEKUCHA KIKOMBE KINGINE!!

Baada ya Babu wa Loliondo kuvuma kwa kasi ya ajabu tukasikia wa Rombo (fundi baiskeli) bahati mbaya hakuvuma!!!,kaja dogo wa Mbeya Mabatini, mara dada wa Tabora wote bei ya KIKOMBE ILIKUA Tshs 500/= na sasa ni Dada wa Morogoro!!. Tena huyu kaja na 'sale' KIKOMBE 200/=. Toka tusikie KIKOMBE  watu Kibao wapo bize na Vikombe sasa mie sijui  ngoja tuone mwisho itakuwaje HUU MWAKA WA VIKOMBE, inatishaa..


Kwa habari zaidi tembelea kero nyingi blog hapa: http://keronyingi.blogspot.com/2011/03/breaking-news-kuna-dada-wa-mji-kasoro.html

29 March, 2011

WHAT GOES AROUND COMES AROUND (UNAWEZAJE KUTUNZA UUAJI WA NAMNA HII?)

Daaah nilikua naperuzi blog mbali mbali pamoja na kusoma vitu vingi hiki kimenigusa na nina shangaa mtu unawezaje kufumbia macho ama kujishauri kuhusu mtu anaye ambukiza watu ukimwi kwa makusudi? ''What goes around comes around'' huwezi jua huyo dada anatembea na watu gani huko aliko usikute hata boyfriend wako ashampitia na kama bado iko siku.Chain ya ukimwi ni kubwa jamani tusipoteze muda kuokoa maisha ya wenzetu inapotokea kitu kama hiki.Mtu huwezi sema aah mbona mimi hainihusu huwezi jua huo UKIMWI  wa rafiki yako ukazunguka hadi kukufikia wewe.

Si jambo la busara kufumbia macho mtu yeyote anaye ambukiza watu virusi vya ukimwi tena kwa maksudi, kwa mtindo huu Tanzania bila ukimwi itawezekana kweli? Tena huyu msomi kabisa anadiriki kujiuliza mara mbili swala zito kama hili.Sasa ambaye hajasoma atafanya nini?

Kwa habari zaidi soma hapa:  http://beautytouchdar.blogspot.com/2010/07/rafiki-yangu-anaambukiza-watu-ukimwi.html#comments

''RAFIKI YANGU ANAAMBUKIZA WATU UKIMWI KWA MAKUSUDI, NIMFANYAJE? AU NIWAAMBIE UKWELI? ''


 Hicho ndio kichwa cha habari yenyewe mtu anaomba ushauri.(tafadhali fungua hiyo blog soma humo inasikitisha sana) Si kwamba ni unyanyapaa lakini kitu kama hiki sio cha kufumbia macho hata siku moja ni uuaji tena wa maksudi ambao hautakiwi kuukumbatia kwa namna yeyote ile.

28 March, 2011

HIVI NDIVYO WENZETU WAKENYA WANASEMA KUHUSU LOLIONDO

Wakenya wataka babu wa Loliondo afungwe kwa kile kinachodaiwa kupotosha watu kwani anajifanya yeye Yesu mponyaji (sijajua wakisikia na ya Mbeya watasema nini!!!!)..Kwa habari zaidi sikiliza hii Video ya kwanza ambayo inataka Babu Mwasapile akamatwe na kufungwa mara moja.Kwa habari zaidi za Loliondo angalia video zinazo fuata kwa hisani ya NTV ya Kenya







Video kwa hisani ya NTV.CO.KE

NAMNA YA KUMKERA MPENZI/MCHUMBA/MKE AU MME

Hivi ni baadhi ya vitu ambavyo vinaweza sababisha kuvunjika ama kutoweka uaminifu katika mahusiano.Mie sio mtaalamu sana katika mahusiano lakini mambo nitayo zungumzia hapa hayahitaji utaalamu wowote hasa hiki kipindi cha utanda wazi.Vitu nitavyo taja ni vya maisha ya kawaida ya kila siku kwa wapenzi,wachumba au wanandoa bila kusahau mchango wa vyombo vya mawasiliano katika kubomoa ama kujenga mahusiano Mfano simu, Internet au mitandao ya kijamii kama facebook n.k .

Ni vitu vya kawaida ila madhara yake makubwa kama hutakua makini.Nimezungumza kwa namna vitu hivyo huweza kukera na ukiepuka utakua kwenye safe side.Ungana nami hapa chini:-
1.Ukitumiwa meseji/barua pepe usijibu au jibu siku na saa utakayo jisikia
2.Ukipigiwa simu na mwenza wako usipokee na hata ukiona missed call usipige,wala text,au kuomba kupigiwa!!
3.Ukipigiwa simu mbele ya mwenza wako nenda mbali ukapokee simu huko ukimaliza rudi na muendelee na kile mlikua mnafanya
4.Simu weka password na futa contact records za kila siku kuanzia msg,calls,etc na jina katika contacts andika jina baya baya lisilo lake mfano Jinga,kidumu, kero,msumbufu,wewe nani,wale wale,mzushi etc
5.Akikupunguzia salio kwenye simu wewe mpunguzie mwingine(mke mpunguzie mwaname mwingine),(mme -mpunguzie msichana mwingine) na baada ya hapo uwe una beep tu hata kama umepunguziwa salio.
6.Mkiwa pamoja matembezini kama wewe mke uwe unaangalia sana wanaume wengine na mwanaume uwe unaangalia wasichana wengine na kutokusikilizana.
7.Usiwe na attention yeyote wanasema ''kila mtu ana shida zake usikilize za mwingine za nini''
8.Kuwa bize na vitu visivyo eleweka mfano kutuma text zisizo isha au kuwapigia watu wengine simu na kuongea umbea wakati mwenza wako anataka kuongea na wewe.
9.Uwe mchafu mchafu usiye jipenda
10.Uwe umenuna kila mara
11.Zima simu kila ukiwa na mwenzio ili usipigiwe na yeyote na kuiweka mbali na mlipo.
12.Ukiwa nae sifia (mme-sifia wanawake wengine eti wazuri na wana adabu), (mke-sifia wanaume wengine mbele yake)
13.Toa siri zenu zote watu wajue (hata za chumbani!!)
14.Kusemana mbele za watu au kutukana mwenzio kwa dharau
15.Uwe unachelewa kurudi nyumbani bila sababu za msingi (kwa wanandoa)
16.Kunywa sana ukifika nyumbani tapika (kuny*) kila mahali na usisafishe!!
17.Ukiongozana na mpenzi wako mtambulishe kama rafiki yako kwa rafiki zako
18.Mkiongozana kila mtu atembee pekee yake kama hamjuani vile.
19.Kama mna kawaida ya kwenda club basi kila mtu acheze na mtu anayetaka cheza naye na kwa kujiachia!
20.Kuwa mtu unayetaka kuheshimiwa bila kuheshimu kisa your somebody kazini,ktk biashara,n.k
21.Ukiwa na mwenza wako zungumzia zaidi past relations  zilivyo kua na namna mlivyokua mki enjoy na mengine mengi.

NB.Si kila mtu anachukulia sawa jambo fulani kwahio kuwa makini na tabia zako au mambo unayo fanya.Ukiepuka hii utakua umeepuka mengi.Pia nitafurahi kama kuna mwenye zaidi kwani haya ni baadhi tu ya mambo yanayo kera.Kama una zaidi unaweza acha kwenye comments.Pamoja!

27 March, 2011

A LITTLE BIT OF HISTORY -STUDENTS I'M HERE FOR YOU!!!

•What two African countries were never colonized?
Ethiopia and Liberia.

•What are the African countries colonized by Britain?

Sudan, Egypt, Union of South Africa, and Zimbabwe, to name a few. The rest are on this map: http://www.africainstitute.com/map_colonization.htmlbelend

•What African country was colonized by Spain?

In africa spain colonized a little region in norther Morocco known as Rif, another little bit in southern Morocco known as Ifni, the Western Sahara and Equatorial Guinea.

Read more: http://www.wiki.answers.com/Q/Which_African_countries_were_never_colonized#ixzz1HkmKJD5w

America was colonized by Britain up to its independence in 1776, where is America now???..puzzled? if no/yes me too!!..please Tanzania wake up.I hope one day we'll stand firmly,arrogantly,proudly with all the instincts saying we are peacefully happy and will always be.God bless Tanzania.

23 March, 2011

BRAND NEW ORIGINAL LAPTOP FOR SALE

         ***** The Cheapest & Quality Laptop in Town*****



 Brand:-------------------Toshiba (Made in the UK)
Operating system............Genuine Windows 7 Home Premium.
Processor -----Dual core AMD Athlon™ II X2 P360 Processor - 2.3GHz,
                                                                                                   - 1MB L2 Cache
                                                                                                   - 1.8 GHZ HT

Screen type----------------------------Widescreen LCD

Screen size------------------------------15.6"
Hard drive ----------------------------640GB
Ram-------------------------------------4GB

Disk drive--------------------- ----DVD Super Multi writer drive (Double Layer)
Memory card reader ------1 × Multi-Card Reader (supports SD™ Card up to 2 GB,  miniSD™/microSD™ Card with adapter up to 2 GB, SDHC™ Card up to 32 GB, SDXC™ Card up to 64 GB and MultiMedia Card™ up to 2 GB)

Webcam--------------------Integrated VGA Web Camera with built-in microphone

Battery ----------------Technology : lithium-ion Maximum life : up to 4h10min (Mobile Mark™ 2007)
Software included -----Toshiba Disc Creator

                                     -Toshiba User Manual
                                     -Supervisor Password Utility (Finger Scanner)
                                     -Toshiba Assist
                                     -Chicony Camera Assistant Software
                                     -Toshiba Face Recognition
                                     -Toshiba Value Added Package ---(Toshiba Power Saver, Toshiba Zooming Utility, Toshiba PC Diagnostic Tool, Toshiba Flash Cards, Toshiba Components Common Driver, Toshiba Accessibility, Toshiba Button Support)
                                   -WildTangent Games Console
                                   -Toshiba Photo Service
                                   -Toshiba Recovery Media Creator
                                   -Nero 9 Essentials
                                   -Nero BackItUp & Burn Autobackup Essentials
                                   -Microsoft Office 2007 (Full Package Installed)
                                   -Connectivity Doctor
                                   -Config Free™
                                   -Toshiba utilities and drivers
                                   -AVG Anti-virus (Full Package Installed)

Weight---------------2.3 kg
Colour-----------------Black
                                      
                                             For Inquiry call now :0714 67 17 54 or email  rijaki@ymail.com

PROPER SCRUTINY UNDERWAY ON STUDENT VISA INTO THE UK

The rules for student visas into the UK are to be much tougher - after fears that this route of entry is being used dishonestly. The Home Secretary Theresa May said student visas were being abused and "too many were here to work and not to study". To start with, she announced plans to cut quarter (80,000) of the current number of students entering the UK.
Mrs May told the House of Commons that the misuse of student visas had become a "symbol of a broken and abused immigration system". On the other hand Shadow Home Secretary Yvette Cooper warned that rules must not damage an industry worth £5bn a year.
Accordingly, to tighten the process language rule will be used. Students must be able to speak English. Besides that, students must at least be able to describe their courses to be pursued. That according to her will make the most in the best interests of legitimate students only.
Also tighter regulations will be introduced on the dependants of students to join them in the UK plus less flexibility in the number of years that overseas students can spend after graduation.
On top of that overseas students will have limits on hours of paid work.


22 March, 2011

NAMNA YA KUFELI SHULE KWA MAKUSUDI



                                                            ??????


1.Usiwe na ratiba ya kujisomea

2.Usiende maktaba kusoma wala kujikumbusha ulivyo soma darasani kwa muda wako wa ziada.

3.Usisome vitabu, wewe soma tu 'summary' za notes na kamusi ili ujue tu maneno magumu ya kuwatishia wengine kua msomi na lugha ina panda kwa sana.

4.Susia vipindi ukijisikia uvivu lala tu wakati wenzio wako darasani au safiri safari ya mbali kula starehe huko

5.Kesha sana kila siku lala saa tisa usiku au kumi kabisa alfajiri wakati shule unatakiwa kuamka saa moja asubuhi kila siku.

6.Nenda club mara nyingi iwezekanavyo kama vipi kila siku ukiweza.
7.Kuwa mlevi na mwingi wa wanaume/wanawake wakati uko masomoni.

8.Wakati mwalimu anafundisha wewe piga story na rafiki yako na kubadirishana vi memo chini chini vya kuchekesha au cheza game kwe simu au chochote chenye game.

9.Ukipewa mtihani anza kufanya bila kusoma maelekezo kwanza.

10.Kua mtovu wa nidhani na unaye taka ugomvi kila siku na uende darasani ukiwa umelewa.

11.Usisome wakati unategemea kufaulu mtihani kwa miujiza.

12.Usisikilize walimu wako au walezi/wazazi wako.

13.Uwe mchelewaji kwenda  kwenye vipindi shule na uwahi kuondoka kwenda nyumbani/bwenini

14.Uwe mpenda sifa,mjuaji wa kila kitu, majivuno ya kwenu mna pesa shule sio ishu.

15.Mwalimu anapo fundisha usichukue notes kaa tu muangalie kama kideo na ongezea kusinzia ikibidi.

16.Usijali nafasi unayoshika baada ya mitihani yako 'after all is just a number!!

17.Waambie wenzio 'wametumwa na kijiji kuja kusoma ndio maana wanajituma sana' na wewe kusoma kwako sio ishu sana, after all shule ikishindikana unaweza kuwa konda wa magari ya''baba/mama,mjomba,shangazi, baba mdogo nk''

18.Ukipewa maswali ya kujibu usifanye yaangalie tu na hisabati soma kama notes usi kokotoe hata moja 'after all ni ugonjwa wa taifa' na kama mmepewa kazi ya kundi wewe usishiriki chochote endelea na mambo yako upate 'marks' za bure

19.Wakatishe wenzio tamaa ''kufauru darasani sio kufauru maisha'; ' wasomi mbona wengi halafu wote choka mbaya tu (kusoma sio dili)

20.Ukiwa hujaelewa darasani usiulize kisa utaonekana mjinga!

NB.Yaliyo tajwa baadhi  hapa juu kama yataepukika lazima ufauru shule (i.e kuanzia msingi mpaka vyuoni), hata hivyo sio lazima haya tu yakufelishe yako mengi zaidi yanayoweza fanya mtu afeli shule na pia si kila mtu anafeli akifanya haya kwani kuna sababu mbalimbali zenye athari tofauti baina ya mtu na mtu.

Je una la ziada? Nitafurahi kusikia kama kuna mengine ambayo yana mfelisha mwanafunzi akiwa shule/college/chuo.

21 March, 2011

LIBYA SI SHWARI TENA!!

Baada ya vikao kadhaa vya baraza  la usalama la umoja wa mataifa kutafuta mstakabali wa machafuko nchini Libya ambapo China na Russia zilionyesha waziwazi kutoshiriki na lolote huko Libya.Marekani haikua tayari bila tamko la baraza la umoja wa mataifa ambalo limepita na Marekani iko mstari wa mbele kushambulia maeneo muhimu yanayosadikika kutunza silaha inchini Libya.Rais wa Marekani ambaye yupo ziarani nchini Brazil ametoa idhini ya jeshi lake kuendesha mashambulizi ya kijeshi inchini Libya.


Jengo la kijeshi lilio haribiwa Tripoli-Libya

Shambulizi la kwanza limeripotiwa kuharibu jengo kubwa la kijeshi na kuangusha ndege 4 za kijeshi za jeshi la Gaddafi.Hata hivyo Gaddafi ametangaza kuangusha ndege yeyote itayo onekana juu au eneo lote la Mediteranian sea zikiwemo ndege za abiria huku akitahadharisha kua atatumia silaha nzito ambazo hajaanza kutumia na ameahidi kushinda mashambulizi ya wana muungano wa umoja wa mataifa wakiongozwa na USA,UK & FRANCE.Vita kwa namna yoyote si nzuri Mungu awasaidie.


   
                                       Kituo kimoja cha ulinzi wa anga Libya kikiwa kinawaka moto baada ya kulipuliwa na majeshi ya muungano wa UK,USA na FRANCE.

Kwa habari zaidi soma hapa
>> http://abcnews.go.com/International/libya-international-military-coalition-launch-assault-gadhafi-forces/story?id=13174246

>> http://abcnews.go.com/wnt/video/special-report-target-libya-president-politics-war-obama-military-13175613&tab=9482930&section=1206853&playlist=1363340

17 March, 2011

UN YASHINDWA FIKIA MWAFAKA KUHUSU LIBYA



UN


UN mpaka sasa imeshindwa kufikia muafaka kuhusiana na machafuko ya ksiasa nchini Libya.Hali hio imejionyesha baada ya baraza la usalama la umoja wa mataifa kumaliza kikao jumatano ya tar 16/03/2011 bila ya makubaliano dhidi hatua za kudhibiti ghasia zinazozidi kupamba moto mpaka hivi sasa. Wakati huo huo mtoto wa Gaddafi Seif al-Islam amesema ndani ya masaa 24 watakua wameshachukua jimbo lililo chini ya wapinzani (Benghazi)  na wapinzani hao wameambiwa waondoke Libya.
(Voice of America)

Yafuatayo ni maoni ya nchi baadhi toka baraza  la usalama l a umoja wa mataifa:
Ufaransa & Uingereza UN itumie   jeshi kuzuia machafuko Libya
Italia:Haitahusika kama jeshi litatumika kutuliza ghasia Libya
Slovania: Kuingia kijeshi Libya ni hatari zaidi
US: Tupo tayari kuingia kijeshi Libya kwa mgongo wa UN.
China:Kuingia kijeshi si haki

Kikao kingine  cha dharura  cha baraza hilo  kukaa leo Tar 17/03/2011     kujadili hitima ya ghasia  inchini Libya

NANI HAPA KAIBA KWA MWENZIE??!


Kati ya Daddy Owen-Kupe De Kalle (Tobina) ft Kerah  hapa juu na
Coupe Decale (Alaji)  hapa chini nani kaiba au ni mixtape?.Nahio 'Tobina' ni Gospel na 'Alaji' ni dansi!!!..pamoja na hayo je nani unadhani kaitendea haki beat ya nyimbo hii? Mie naona wa 'Tobina' ndio zaidi japo wamejiachia kama dansi vile.Mwanzo nilipo sikiliza nikadhani ni dansi, mara ya pili ndio nika gundua ni Gospel baada ya kusikia ''ayo lele kuna moto, kuna waka kuna moto, yesu mwokozi'' Sikiliza na wewe.

15 March, 2011

KATUNI YA LEO..

KWA BABU HUDUMA KAMA KAWA HABARI ZAIDI KUPITIA ITV & STAR TV

                                          Video toka ITV-Loliondo

                                        Video toka Star Tv--Loliondo

11 March, 2011

JAPAN YAKUMBWA NA TSUNAMI

Japan imekumbwa na tetemeko kubwa la bahari maarufu kama Tsunami ambalo limesababisha uharibifu mkubwa wa mali na maisha ya binadamu mapema leo.Tetemeko hilo  kubwa kiasi cha 8.9 magnitude limeripotiwa kuathiri sehemu kubwa ya maeneo ya pwani kaskazini mashariki mwa Japan ambako mamia ya watu wana hofiwa kufa kwa kuangukiwa na nyumba na mafuriko makubwa ya maji yaliyo tapakaa toka baharini na kubomoa nyumba,kuzamisha magari,meli na kusababisha moto mkubwa baadhi ya maeneo.

Tetemeko hilo  la kihistoria limepelekea kuzimwa kwa mitambo minne ya Nuclear ambayo hutumika kufua umeme wa Gigawatts 11.Halihiyo imepelekea maeneo mengi kuwa bila umeme.Japan  ni moja kati ya nchi zinazo zalisha umeme kutumia Nuclear na asilimia 30 ya umeme wake hutokana na nishati hio.


                            (Ramani ya Japan)


Wataalam wa mitambo hio wame tahadharisha kuhamisha watu wote karibu na mitambo hio iliopo pwani ya Japan maeneo ya Fukushima na Fukui kwani tetemeko limeathiri mitambo hio na kuweza kupelekea uwepo wa mionzi inayo athiri watu au hata kusababisha vifo.Kudhibiti hilo marekani imeripotiwa kupeleka kipozeo cha mitambo hio baada ya kilichokuwepo kuharibiwa kutokana na tetemeko hilo.

Kwa picha zaidi na Video toka BBC  bonyeza kwenye link :http://www.bbc.co.uk/news/world-asia-pacific-12709847. Pia videoa toka RT angalia chini

                                                                 RT (2 mins Video footage  11/03/2011)

10 March, 2011

50 INCH PANASONIC PLASMA TV OFFER


Brand new Original Panasonic plasma Tv 50 Inch (127cm) for sale ***Made in the United Kingdom (UK)*** Very cheap!!!!For Serious inquiry please email: rijaki@ymail.com OR Call: 0653624150;Location: Dar es salaam.Delivery:Free (In Dar es salaam only
 

Product Features and Technical Details
Product Features

• VIERA HD Ready 50-inch Plasma TV
• 100Hz Double Scan for ultra-smooth picture quality
• Dynamic Contrast 2,000,000:1
• VSmart Networking with VIERA Link and VIERA Image Viewer (integrating Photo and Video)
• Game Mode, V-Audio Surround

TV Tuner:
Integrated Tuners: PAL-I, DVB-T
Tele text Reception: 1000P Level 2.5, FASTEXT/LIST

Display
Screen Size: 50" (127 cm) diagonal
Panel: G13 Progressive HD Plasma Display Panel with Tough Panel
Viewing Angle: Viewing Angle Free
Resolution: 1,024 x 768 (16:9)
Applicable Scanning Format:
FULL-HD 1125: (1080)/50i, 1125 (1080)/60i, 1125 (1080)/24p (HDMI only), 1125 (1080)/50p (HDMI only), 1125 (1080)/60p (HDMI only)
HD: 750 (720)/50p, 750 (720)/60p
SD: 525 (480)/60i, 525 (480)/60p, 625 (576)/50i, 625 (576)/50p
Contrast Ratio (in dark surroundings): 2,000,000:1 Dynamic
Moving Picture Resolution: 720 lines
Intelligent Frame Creation: 100 Hz Double Scan
24p Smooth Film/Plaback Plus/Playback: 24p Playback
Shades of Gradation: 4,096 equivalent steps of gradation
Deep Colour (10/12-bit): yes
3D Colour Management: yes
Picture Mode: Dynamic/Normal/Cinema/True Cinema/Game/Photo
Vreal: Vreal 5

Sound
Speakers: 2 x 10 watt 2 Speakers
Sound Mode: Music/Speech/User
Virtual Surround: V-Audio Surround
Dolby Digital Out/CoNEQ: Dolby Digital

Input/Output
CI (Common Interface)*: yes
VIERA Image Viewer: yes (AVCHD/SD-VIDEO/JPEG playback)
HDMI Input/ Support Feature: 3 (1 side, 2 rear)/ Audio Return Channel (Input 2)
Composite Video Input: AV3: RCA phono type x 1 (side)
Audio Input (for Video): AV3: RCA phono type connectors (L, R) (1 set, side)
Component Video Input: RCA phono type x 3 [Y , PB, PR] (rear)
Audio Input (for HDMI, PC, Component) RCA phono type connectors (L, R) (1 set, rear)
21-Pin Input/output: AV1: AV In/Out, RGB In, Q-Link (rear) / AV2: AV In/Out, S-Video In, RGB In, Q-Link (rear)
Analogue Audio Out: RCA phono type connectors (L, R) (1 set rear)
Digital Audio Output (Optical): yes
Headphone Jack: 1 (side)
Features
EPG: yes
VIERA Tools: yes
VIERA Link: yes (HDAVI Control 5)
Multi Window: PAT
C.A.T.S. (Contrast Automatic Tracking System): yes
Game Mode: yes
Q-Link: yes
Off Timer: yes
Child Lock: yes

General
Wall mountable: yes
Power Save Mode: yes
Power Supply: AC 220 - 240 V, 50/60Hz
Rated Power Consumption: 265 W
On mode Average Power Consumption: 201 W
Standby Power Consumption: 0.4 W
Dimensions (W x H x D) (w/o stand): 1,218 x 769 x 93 mm
Dimensions (W x H x D) (with stand): 1,218 x 814 x 401 mm
Weight (w/o stand): 31.5 kg
Weight (with stand): 33.5 kg
Boxed product : 40kg
Wall Bracket: TY-WK4P1RW (not included)
Remote Control:Yes (included)

09 March, 2011

YALIYO JIRI-LOLIONDO



                                                ITV  na Taarifa kuhusu kinacho endelea Loliondo



Hali livyo hivi sasa Loliondo kwa babu.

Hakika huyu babu anahitaji msaada wa haraka maana pamoja na watu kwenda wakitembea wenyewe, kuna wale wagonjwa walio bebwa ambao bila shaka hali zao sio nzuri.Si hivyo tu pia hali ya usalama kufuatia kugombea huduma kunaweza zua jambo lingine la hatari.Kila mtu anataka kuishi, kila mwenye mgonjwa angependa mgonjwa wake atibiwe mapema iwezekanavyo ila kwa uwingi huu wawatu hakika huyu babu hataweza kumudu akiwa hana msaada  wa ziada kwani watu hawataweza vumilia kulala nje kila siku.Si hivyo tu kuna wagonjwa ambao kwa msongamano huo wa watu lazima watapoteza maisha.Serikali ichukulie jambo hilo uzito wa ziada ikiwa ni pamoja na kuhakiki ukweli wa tiba hio. Ni hayo tu kwa leo.

08 March, 2011

BABU ANAYE SADIKIKA KUTIBU UKIMWI AFURISHA WATU-ARUSHA

Babu mmoja kwa jina Ambilikile Mwasapile (76) wa Loliondo wilayani Ngorongoro mkoani Arusha amejipatia umaarufu wa ghafla baada ya kugundulika anatibu magonjwa lukuki ukiwemo UKIMWI.Babu huyo ambae inasaidikika ni mchungaji mstaafu wa kanisa la KKKT-Loliondo amesema mwanzo ilikua ni ndoto ambayo amekua akiiota toka mwaka 1991 ambayo Mungu amemuagiza aponye watu.Ndoto hio imejirudia rudia mpaka Augusti mwaka 2010 ambapo aliamua  kuanza kutoa tiba rasmi kwa gharama ya sh.500 tu.

 

Mpaka sasa maelefu ya watu mbalimbali,vijana kwa wazee, wanaume kwa wanawake wamekuwa wakienda kwa mzee huyo kupata tiba na baadhi wamekili ni TIBA HALISI.Mpaka sasa ni kama kitenda wili machoni pa watu kila mtu akiuliza ni kweli au sio kweli.Kwenye mitandao mbalilimbali kama facebook,blogs,webisites na chatrooms  gumzo ndo hilo japo bado hawaamini kama ni kweli na wanasema kama ni kweli na wao wataenda

 

Kwa walio ona foleni ni kubwa kupita maelezo katika kufata tiba hio ya asili na huenda babu huyo akavunja rekodi ya utojai tiba asili nchini Tanzania tena kwa muda mfupi. Kama utavyo ona picha hapo chini watu ni wengi sana kama nilivyozitoa Facebook.

 

Siku zote mimi huwa nasema kwa watu wa karibu UKITAKA KUJUA KAMA KUNA WATU WANAUMWA NENDA HOSPITALI NA UKITAKA JUA KAMA WATU WANAKUFA NENDA MAKABURINI.Bila hivyo hutajua labda kama anaye umwa ama kufa ni ndugu ama jirani au wale ambao utaona ama kusikia kupitia vyombo vya habari.

 

        Msafara kwenda kwa babu


    Babu akiwa amezungukwa na watu waliofata tiba pamoja na kushangaa

           msafara ndio kama hivi ( babu asababisha foleni)

07 March, 2011

LIVE TOKA ENEO LA TUKIO..

Katika kupita pita kupata habari hapa na pale nikaja kutana na habari ya mada kuhusu  urembo wa wasichana wakitanzania dhidi ya wale wanaijeria kupitia http://u-turn.co.tz/index.php?start=10. post ya tarehe 01/03/2011. Mada hio iliambatana na pichaa kadhaa za wasichana wa kitanzania yamezaa maoni lukuki yaliyo katika mtindo wa kubishana/kujibishana tena kwa maneno makali. Mpaka sasa haijajulikana nani ameanzisha malumbano hayo makali  pamoja na kutuma picha kwa blogger aitwae Linda wa Nigeria.

Wengi wanasema pengine imekua gumzo kwa mshindi wa BBA (Kevin-Nigeria) kumuoa Mtanzania (Elizabeth) wakiuliza kwani Nigeria wasichana wazuri hakuna? kwenye comments za wanaijeria wakaka wanasema wadada wakitanzania hujipendekeza kwao kwa uzembe wakutaka vya bure na wao ndio wanawachukua ila si kwamba ndio wazuri.Mimi sijui ukweli ndio upi zaidi ya kusikia wasichana (Baadhi) wakitanzania kuwasifia wanaijeria ndio wanaume wa ukweli na wanajua kujali (mimi sina maoni juu ya hilo)

Ukisoma maoni yaliyo tolewa wameitukana hadi Tanzania kama nchi (Too bad) hasa katika swala zima la umasikini na kwamba wengi wetu ni vihiyo,washamba,lugha haipandi na masikini wakubwa.Hata hivyo wa kaka wa kinaijeria wamesema kuwa wasichana wao ni wazuri kupita wakitanzania ila kwakua hawa wa Tanzania ni cheap ndio huwachukua.Wakati huo huo wasichana wakinaija wamesema (kupitia maoni) kua huyo aliye olewa na mume wao (yaani kaka wa kinaija) basi watakula naye sahani moja!

Malumbano hayo ambayo hayana miguu wala kichwa yamezaa maoni mengi  kupita kawaida katika blog hio kwa kulaani hio mada ya kulinganisha kazi ya Mungu (ambayo siku zote haina makosa) na kupelekea kila mmoja kwa nafasi yake kujitetea  tena kwa hasira na Lugha kali.

Blog  hii inalaani yeyote aliyepelekea kuazishwa kwa mjadala huo duni na kutoa wito wa kutoa mada za kujadili mambo ya msingi na maendeleo na sio 'Urembo/beauty' ambao uko subjective kwa kiasi kikubwa kwani kila mmoja anaweza kuwa na mtazamo tofauti katika Urembo wahenga walisema 'Beauty is according to the eyes of the beholder'. Kwahio tujadili mambo mengine sio haya yanayo lete mabishano yasiyo na umuhimu.

 Sitaki kuongea mengi ili kuona mjadala ulivyokua na maoni ambayo mpaka naandika hapa yamefika 134 ingia hapa: http://lindaikeji.blogspot.com/2011/02/are-tanzanian-women-more-beautiful-than.html

Pia ukitaka ona post na comments za u-uturn  kuhusiana na mada hio hio na comments za watanzania ingia hapa: http://www.u-turn.co.tz/index.php/kwanza/1588-ohoooo-wanaigeria-wanatutafuta#JOSC_TOP

03 March, 2011

KUMBE WIZI WAHITAJI UBUNIFU MKUBWA KIASI HIKI?

I just hope this article will be useful to most people wale wanao tumia internet kwa namna moja ama nyingine.Kwa muda sasa nimekawia kutoa post yenye kuhusu athari mbali mbali while surfing on the internet.Lakini nimeona nirudi tena kwasababu ya umuhimu wa jambo lenyewe.Kama mtumiaji wa Internet ni lazima utambue athari hizo nakua makini wanapo tumia tekinolojia hii ya mtandao ambao kwasasa kuna wizi wa hali ya juu.

Pamoja na mimi mwenyewe kutumiwa meseji zisizo pungua 100 za kutatanisha kwa siku.Mfano wa email ni zle za ''umeshinda million moja pounds (£ au $) toka coca cola au British national lottery etc; au wanasema kuna pesa za urithi nisaidie kuziokoa bank ukiwa kama mdhamini wangu'' Baada ya ujumbe huo utaambiwa kuna percentage itakua yako ikiwa hiyo pesa itatoka.

Kuna pia mbinu kama hii mfano nimewaletea hapa chini ni kama vile ananitaka.Actually kuna email address moja ambayo siitumii officially huwa na reply hizi email nione reaction basi wanatuma picha za wasichana wazuri kunitega, mwisho wa siku anakwambia yuko mji jirani na unako ishi yuko stranded mtumie pesa kidogo ili aje kukutembelea kwani pesa imemuishia.Sasa huyu mtu kwakua kuna google translator amediliki kutumia google translation ya barua ya kiingereza kwenda kiswahili just because anajua natumia kiswahili ili anipate.Bahati mbaya amelamba jokeri.

So tuwe makini usidhani ndio bahati imekudondokea utaibiwaaa!!.Kuna wale tunaopenda nunua magari na vitu vingine online
KUWENI MAKINI NA KAMPUNI UNAYO NUNUA, KUNA KAMPUNI NYINGI FAKE ZIPO ONLINE NA HAZINA PHYSICAL OFFICE AND ALL TRANSACTIONS ZIPO ONLINE.ZINA FULL CONTACT ADDRESS LAKINI NO FACE TO FACE TRANSACTION.MPAKA SASA NIMEOKOA WATU ZAIDI YA 10 AMBAO TRANSACTION ZAO ZILIKUA FAKE NA AT LEAST WOTE WALIKUA LAST STAGE YA PAYMENT THROUGH BANK CARDS (INTERNET BANKING).MFANO MTU ANASEMA ANAUZA GARI HALAFU CONTACT NI VIA EMAILS PEKE YAKE HIO JUA FAKE STRAIGHT AWAY. NITALETA TRICKS NYINGINE PUNDE.

MOJA NILIYOTUMIWA MIMI HII HAPA:

Hi! Mimi ni miss Lisa
jinsi wewe! matumaini wewe ni faini na katika hali ya ukamilifu wa health.I safari kwa kupitia profile yako juu (dinahicious.blogspot.com) na i kusoma na kuchukua riba juu yake, kama huna akili i kama wewe kuwasiliana na mimi kwenye hii ID (lisa.samuel1@yahoo.com) ili kwamba naweza kukutumia picha yangu OK matumaini ya kusikia kutoka kwenu hivi karibuni, nami kuwa kusubiri kwa barua yako kwa sababu labda tunaweza kuwa rafiki mwema anyway i nitakuambia zaidi wakati wasiliana nami kwenye email yangu lisa.samuel1@yahoo.com

my Language is English====================

Hi! I am miss Lisa
how are you! hope you are fine and in perfect condition of health.I went through your profile on (dinahicious.blogspot.com) and i read it and took interest on it, if you don't mind i will like you to contact me on this ID (lisa.samuel1@yahoo.com) so that i can send you my photo OK hope to hear from you soon, I will be waiting for your mail because maybe we can be a good friend anyway i will tell you more when you contact me on my email lisa.samuel1@yahoo.com

01 March, 2011

SIKILIZA HOTUBA YA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA MH JAKAYA KIKWETE

Gaddafi azidi kuishangaa dunia..

Kanali Gaddafi anazidi kuishangaa dunia kwa kumshinikiza ajiuzulu eti wananchi wamemchoka.Gaddafi anauliza ajiuzulu kutoka wapi wakati yeye sio Mfalme wala Rais na pia watu wake wanampenda kiasi cha hata kufa kwaajili yake?.Amesema hayo alipo hojiwa na BBC huko Libya.Ameongeza kuwa wanao andamana ni Al-Qaeda na watu walio wengi ni mashabiki wake na si vinginevyo.Amemalizia kusema Dunia haiijui Libya ni nini na ina serikali ya namna gani ndio maana wana muharibia.''Libya watu wangu wananipenda, hao wengine ni Al-Qaeda'' Gaddafi alisema.
(BBC)
Zaidi soma hapa:http://www.bbc.co.uk/news/world-africa-12603259