10 April, 2012

KUMBE POLISI NAO HUIBIWA!!!

Habari toka majuu (Kwa Malikia/UK aka Ukerewe) zinasema maelfu ya pauni za Uingereza aka Great Britain Pound (GBP) yaliyokua mikononi mwa polisi yaibiwa. Pesa hizo ni zile ambazo zilikamatwa kutokana na upatikanaji wake kuhusisha njia ya udanganyifu na kuhifadhiwa katika ghala yenye ulinzi mkali katika kituo kimoja cha polisi wakati uchunguzi zaidi ukiendelea. Watu watatu walitiwa hatiani kuhusishwa na sakata hilo.Hata hivyo pesa hizo kiasi cha 113,000£ zapotea katika mazingira ya kutatanisha.Uchunguzi unaendelea na hakuna polisi wala raia aliyetiwa hatiani kutokana na upotevu huo..Inashangaza eti pesa ikaibiwa kituo cha polisi!!.Hivi polisi hazina bank accounts?.Kweli Duniani kuna mambo!!

Kwa habari zaidi soma HAPA

No comments: