19 May, 2011

VIJISENTI VINAPOSHINDWA KUKUSAIDIA..

Mkurugenzi mkuu wa shirika la fedha duniani (IMF) bwana Dominique Strauss-Kahn ambaye pia ni mwanasheria,mwanasiasa na mwanauchumi wa kifaransa amewekwa jela Marekani kufuatia madai ya kutaka kumbaka mhudumu wa Hotel (Hotel Maid).Baada ya kukamatwa na kufikishwa mahakamani kufuatia kitendo hicho bwana Strauss-Kahn kupitia mwanasheria wake aliomba aachiwe kwa dhamana ya (vijisenti)  Dollar Million moja ($1m) mahakama ilikataa dhamana hio na kumrudisha rumande.


                                       Aliyekua mkurugenzi wa IMF-Dominique Strauss-kahn 

Kufuatia skendo hio mkuu huyo wa IMF amelazimika kujiuzulu wadhifa wake ambapo Umoja wa nchi za Ulaya (EU) wamesha tangaza kinyang'anyiro na wagombea wa awali ni kama ifuatavyo:-

  • Mohamed El-Erian, Egypt

  • Stanley Fischer, Israel

  • Gordon Brown, UK

  • Kemal Dervis, Turkey

  • Peer Steinbrueck, Germany

  • Montek Singh Ahluwalia, India

  • Christine Lagarde, France

  • Agustin Carstens, Mexico

  • Trevor Manuel, South Africa

  • Axel Weber, Germany
  • ETI JUMAMOSI TAREHE 21/05/2011 MWISHO WA DUNIA???!!

    Imeripotiwa kutokea wahubiri wa kidini jijini New York-Marekani kufuatia wanacho dai mwisho wa dunia ni tarehe 21/05/2011 ambayo ni siku ya Jumamosi.Wahubiri hao ambao wamekua wakifanya kazi hio bila kuchoka wametoa vielelezo mbali mbali kuthibitisha tukio hilo.Zaidi wamedai tukio hilo si lazima litokee wakati mmoja duniani kote kufuatia kutofautiana masaa lakini lazima iwe tarehe iliyo tajwa!!

    Ni matumaini yangu hayata tokea yale ya Kibwetere wa Uganda kuchoma moto waumini wake wanao sadikika  kufika 1000 ndani ya kanisa la '' Amri kumi za Mungu'' eti mwisho wa dunia umefika na kubaki yeye na bosi msaidizi wake  Bi Credonia Mwerinde nje mnamo Machi 17 mwaka 2000.Hata hivyo mpaka sasa haijulikani kama Kibwetere  na mwenzie wapo hai na polisi wa Uganda kwa kushirikiana na wale wa kimataifa (Interpol) bado wana mtafuta Kibwetere popote alipo Duniani. Pamoja na kua na maswali mia nane kidogo mie yangu macho!!

    Kwa habari zaidi soma hapa:http://uk.news.yahoo.com/preachers-prophesying-end-world-york-000338169.html

    Zaidi kuhusu Kibwetere soma hapa:http://www.culteducation.com/kibwetere.html