12 June, 2011

CHANGAMOTO YA LEO

Hakika kwa mtu ambaye hajui mazingira ya elimu tuliyonayo Tanzania hususani vijijini hawezi amini mazingira kama haya, kama haitoshi anaweza dhani Haki elimu wanataka kuiumbua tu serikali lakini huu ndio ukweli wenyewe. Mazingira ya kusomea sio mazuri kabisa katika shule nyingi hata walimu wanavumilia tu jamani  haya mazingira sio kabisa. Darasa utadhani gofu?

Ni imani yangu serikali inaona hivi vielelezo basi kipaumbele kiwekwe katika elimu maana huo utakua msingi moja wapo mzuri wa kuondoa umasikini Tanzania kwani kwa mazingira haya sidhani kama kuna mtoto anaweza fauru masomoyake.Na saa nyingine watoto tunawalaumu bure mazingira wanayo somea ni magumu kiasi kwamba shule inakua kama jela matokeo yake wanafunzi kutoroka shule.

Angalia video hii  uone mazingira wanayo somea viongozi wa kesho(sijui ndio lini?)
                  Kwa hisani ya Hakielimutz

Yaani hapa wakisema kila mtu apige picha ya shule ya msingi aliyosoma kuna watu tutashindwa kuonyesha hio picha maana ni aibu hata watu kuiona japokua sasahivi mtu uko kwenye nafasi fulani (Boss).Ni wachache tutafurahia kuonyesha shule tulizosoma.Sasa tunazisaidiaje hizi shule? 

NO CHABO!!!!!