25 June, 2011

WAZIRI AFUNGWA MAISHA RWANDA

Aliyekua waziri wa haki za familia na maendeleo ya wanawake Bi Pauline Nyiramasuhuko afungwa maisha kufuatia madai ya kushiriki katika mauaji ya watusi nchini Rwanda mwaka 1994.Bi Pauline amehukumiwa kifungo cha maisha sambamba na mtoto wake Arsene Shalom Ntahobali ambaye alikua mgambo mashuhuri katika mauaji hayo.Mauaji ya kikabila nchini Rwanda yalianza rasmi mara baada ya kutunguliwa ndege na kumuua aliyekua Rais wa nchi hio JUVENAL HABYARIMANA April 1994 hatimaye kuanza mauaji ya kikabila baina ya wahutu na watusi na kufanya idadi ya waliopoteza maisha hususani kabila la watusi na wahutu kidogo kufikia laki nane (800,000).


Kwa habari zaidi SOMA HAPA