24 May, 2011

FACEBOOK KIBONGO BONGO..

Mimi nimejiunga facebook ili kukutana na marafiki niliopotezana nao muda mrefu mfano Classmates,School mates, University mates,Work/field mates na wengine ili kujuliana hali (kuwasilina kama marafiki), kudumisha  urafiki na kupashana habari zinazo tokea kila mtu alipo kwa wakati ule.Facebook inasaidia kupata marafiki mlipotezana nao hata marafiki wapya na kuwakutanisha

                                                           Facebook logo

Facebook inasaidia kukutanisha watu kwa matukio mbalimbali ya kijamii mfano weddings,parties,kucheza games mbalimbali,kutangaza biashara; kisiasa mfano: mikutano,maandamano; kisayansi mfano: kuendesha mijadala ya kitaaluma na mambo ya teknolojia i.e IT,.Huko Egypt (Misri) Facebook imesaidia kukutanisha watu ambao wameweza hata kuing'oa serikali ya  muda mrefu ya Hosni Mubarak  (14 October 1981 – 11 February 2011) na hata watoto kubatizwa 'Facebook' kama kumbukumbu ya tukio hilo.

Watanzania wengi tumejiunga Facebook kwa kasi kubwa tu,ni vizuri japo sijajua kama matumizi ya huu mtandao yapo sawa! Kwa mtumiaji wa facebook unaweza kua unanielewa.Wengine picha tunazoweka humo ni utata mtupu mfano mtu kaweka picha ya makalio yake tu yakiwa tupu ama nguo inayo onyesha maungo,shanga kiunoni,lips peke yake,au mwili wote ukiwa  na chupi tu,kifua wazi ili iweje? au mtu kaweka picha yenye maneno 'I've the p**sy (ni tusi siwezi andika lote)  so I make the rules' ili iweje?.

Tujiulize tumejiunga facebook ili iweje?.Mtu unakuta yupo ofisini the whole day yuko online (sio idle)  facebook hio kazi anafanya saa ngapi? Mimi nimeona facebook kwa bongo ni 'more of a dating site' je wewe unaionaje? au unaichukuliaje?.Kiufupi madhara ya facebook ni makubwa kuliko, mfano watu wengi wamefukuzwa kazi,ndoa nyingi zimevunjika,watu wengi wameuawa kwa kupitia facebook hasa wale wasio ogopa kukutana mtu usiye mjua,kubakwa,kufungwa, mahusiano mengi yamevunjwa,na watu wengi  sasahivi hufuta (deactivate) akaunti facebook wanapooa,kuolewa ama kugonganisha wapenzi.Be careful na facebook kabla huja umbuka...na pia nijibu......

                                        Wewe umejiunga facebook ili iweje?
                                      Kiraka amejiunga facebook ili......

                                     Ochu anajibu hilo swali msikilize hapa chini




UFUNGUKAJI WA WASANII WETU OVYO!!

Hapa chini ni video ya Clouds Tv 'Take one' 'MTU KATI' na Zamaradi.Angalia vizuri hii Video clip then sikiliza mtu kama msanii ambaye ni kioo cha jamii anapo ongea katika chombo cha habari.Kuna kipengele anasema usanii wake umemuweka karibu na mabinti,imempa mademu,imemuongezea upendo kwa mademu!!! huyu ndio kioo cha jamii!! ...Ninge elewa angesema usanii wake umemuweka karibu na watu SIO MADEMU (HII NI PUMBA).Pia anasema hua anafanya ukauzu kwa mademu wanao mtega kwa kuvaa miwani tinted kwa maana hio ''katufanyia ukauzu Watanzania tunao angalia hii interview kwa kutuvalia hio miwani'' MAELEZO YAKE HAYAJA JITOSHELEZA!!

Si kwamba na 'hate' kwanza simfahamu namsikia tu....Kiukweli ameongea kituko cha mwaka coz movie hawangalii mademu peke yao,aidha kwenye hii interview MNYONGE MNYONGENI HAKI YAKE MPENI.. nimependa kipengele cha matumizi mabaya ya lugha katika movie zetu (movie editors kama wapo wawe makini na kazi yao) na sehemu nyingine zote uozo mtupu na ameaibisha wasanii wenzie (mtazamo wangu)...sikiliza halafu nipe mtazamo wako pia (ni mtazamo tu)

Msikilize Hemed akifunguka hapa chini (Aibu)
(kwa hisani ya Zamaradi Mketema)
                                                         

Vituko vingine vya wasanii angalia hapa: http://www.globalpublishers.info/profiles/blogs/hasheem-thabeet-afanya

SIMBA SC KUVAANA NA BIRMINGHAM CITY FC JULY 7 MWAKA HUU

Timu ya mpira Simba Sports Club ya Dar es salaam kuvaana na Birmingham City Football Club ya Uingereza Julai 7,2011.Hayo yatategemea kuthibitishwa baada ya timu ya wataalamu toka Uingereza kuona kiwango cha uwanja na mazingira kiujumla kimichezo baada ya kukagua tarehe 16/05/2011.Kama mechi hio itaridhiwa Birmingham City ita ambatana na mashabiki  wasio pungua 1000 watakao jilipia gharama za safari na malazi wenyewe wakati timu itajipatia vijisenti visivyo pungua Dola Million 1.2 na kulala hotel nzuri.

                                kikosi cha timu ya simba

Mpaka sasa safari ya BCFC kwenda Tanzania haijathibitishwa baada ya ukaguzi ulio pangwa ufanywe tarehe tajwa hapo juu na pia kutokana na ratiba za mechi za hapa ulaya.Baada ya hayo yote kukamilika ndipo safari itathibitishwa.Pia nimetembelea mtandao wa Simba SC (http://simbasportsclub.co.tz/v3/)  hakuna taarifa yoyote kuhusu mechi hio sasa sijajua mashabaki tutajua nini kinaendelea maana menu zenyewe hazina maelezo yoyote yaani hata menu iko empty: Mfano events,matches,News hakuna kitu-sijui labda nimeingia sio site yenyewe kuna anayejua anipe site halisi please! maana kama ndio yenyewe bado hatupo siriazi kiukweli maana haina cha maana zaidi ya orodha ya viongozi,wachezaji na historia ya timu!!!!!.Angalieni Yanga http://www.yangasc.com/

Anyways, hongereni Simba kama hio mechi itachezwa na nawatakieni ushindi dhidi ya wazungu!.

soma zaidi hapa:http://www.goal.com/en/news/89/africa/2011/05/03/2469421/birmingham-city-officials-to-inspect-facilities-in-tanzania
                          : http://www.birminghampost.net/midlands-birmingham-sport/west-midlands-sports/birmingham-city-fc/2011/04/18/birmingham-city-tanzania-confirmed-as-potential-destination-for-pre-season-tour-97319-28542251/

LIMO YA OBAMA MAARUFU KAMA ''BEAST'' YABUMA ZIARANI IRELAND

Gari moja wapo katika msafara wa Obama  huko Ireland yabuma baada ya kugonga tuta nje ya ubalozi wa Marekani jijini Dublin-Ireland.Gari hilo aina ya Cadillac la Mr Obama lenye jina maarufu kama ''The Beast'' Yaani 'Mnyama' kwa kimakonde lilisekana kubeba wataalamu wa ulinzi katika msafara huo wakati Rais wa Marekani Barack Obama akiwa ziarani nchini humo jana tarehe 23/05/2011.

Umati mkubwa wa watu umeshuhudia tukio hilo 'live' ambapo mlio mkubwa ulitokea baada ya chesis lake kugusa tuta na kushindwa kwenda mbele na muda si mrefu waliletewa gari lingine kuendelea na msafara.


Kama uonavyo kwenye video hapo juu hicho ndicho kilichotokea.Limo/The Beast hilo lina  urefu wa futi 18 na uzito wa tani 8 na upana wa chuma cha bodi wa inch 8 halipitishi bomu wala risasi na lina lina oxygen yake ndani.Rais Obama akiwa ndani ya hilo gari nick name yake inakua Cadillac one na sio The Beast.  The beast inasemekana kua na camera kila kona,shotguns na vingine vingi kwa ulinzi zaidi                               


Mafundi wakinasua The Beast iliponasa



The Beast katika mchoro

(chanzo:dailymail)