28 June, 2011

SULTAN KOSEN MTU MREFU KUPITA WOTE DUNIANI ANATAFUTA MCHUMBA!!

       Sultan Kosen na He Pingping (picha toka the Telegraph)


Pichani juu ni Sultan Kosen ambaye ndio mtu (mwanaume) mrefu kupita wote duniani kwasasa ambaye ameingia kwenye kumbukumbu za guinness toka February 2011.


Sultan ana urefu wa 251 cm (8 ft 3 inch) na uzito wa 168.2kg na amezaliwa 10 December 1982 huko Mardin Turkey (Uturuki).Hapo yupo na aliyekua mtu mfupi kupita wote He Pingping ambaye kwasasa ameshakufa na amekufa akiwa na umri wa miaka 21, urefu wake ulikua  2 ft 5.37 in (74.61 cm)

Sultan alipo ulizwa ni nini matumaini yake baada ya kuingia kwenye rekodi ya watu warefu akajibu ''napenda kusafiri kote duniani, kupata gari ambayo inanitosha na kuwa na watoto'' Sultan anasema anatafuta mchumba hivi sasa kwahio wadada mnaotaka kuolewa jaribuni bahati yenu!!

Kwa habari zaidi soma HAPAHAPA na HAPA