27 June, 2011

ICC YATOA KIBALI CHA KUMKAMATA GADDAFI LIBYA

International Criminal Court (ICC) imetoa kibali cha kukamatwa kwa Kanali Muammar Gaddafi kiongozi mkuu wa serikali ya Libya na wasaidizi wake wakuu kwa kile kilichodaiwa kutumia jeshi la nchi hiyo kushambulia wananchi waliokua wakiandamana kudai haki.Kibali hicho kina ambatanisha watuhumiwa wa karibu na wasaidizi wakuu kabisa wa Gaddafi akiwemo mtoto wake Saif al-Islam Gaddafi  na mkuu wa usalama wa Libya bwana Abdullah al-Sanussi.
                                                          
Muammar Gaddafi


                                                        Saif al-Islam Gaddafi










Habari zaidi

LIBRARY...

Kwa wale wapenda kusoma vitabu hasa unaposomea maktaba haya mambo yapo sana (angalia picha hapo chini).Hata madarasani kuna wadada wanaova nguo ambazo ukikaa kiti cha nyuma yake unaona shanga,nguo ya ndani n.k.Mie hua najiuliza kama msomi ana vaa vile tena akiwa katika mazingira ya kusoma huko mtaani ana vaa vipi na je jamii inamchukuliaje? Je ndio kuishi kisasa au kishamba? Kwani ukijisitiri vizuri unapungukiwa na nini?






Kwa walio soma UDSM pale chini ya mti wanaita mdegree haya mambo ndio usiseme sijui kama kuna mtu anasomea pale anaelewa! labda kipindi cha mitihani ambapo unaweza somea sehemu yenye kelele za kutosha na ukaelewa kama kawaida.Kama mdegree bado ipo mtazamo wangu naona inafaa kwa mijadala ya vikundi ama kupumzika baada au kabla ya kipindi. Mwisho kabisa ushauri wa bure kwa dada zetu vyuoni na popote pale wapatapo ujumbe huu wavae vizuri kusitiri miili yao wengine inakua vigumu kuvumilia unapo ona maungo ya kike na wakati mwingine kama unasoma unaweza shindwa kuelewa unachosoma