19 April, 2012

MZEE WA VIJISENTI WA NIGERIA AFUNGWA MIAKA 13

Gavana wa zamani wa moja ya majimbo tajiri Nigeria, (Delta State) bwana James Ibori afungwa miaka 13 jela.Bwana Ibori alikamatwa mwaka 2010 Dubai kwa makosa ya kujipatia mamilioni kwa njia ya udanganyifu.Mheshimiwa huyo wa ugavana jimbo tajwa kwa miaka ya 1997-2007 baada ya kukamatwa alipelekwa nchini Uingereza ambako alikua ameweka baadhi ya pesa na kununua majumba ya kifahari kwa mahojiano zaidi na polisi mpaka kufikia uamuzi huo wa kufungwa miaka 13 baada ya kuthibitika.Sambamba na hilo mheshimiwa atafilisiwa kwa maslahi ya taifa hilo kubwa kabisa balani Afrika,hususani Afrika Magharibi.


Jeshi la polisi nchini Uingereza lilishangazwa na manunuzi ya gavana ambaye inasemekana mshahara wake ni 4000£= 10Million za  Ki Tanzania kununua nyumba moja kwa gharama ya 2.2 million pounds sawa ma takribani Billion 2 na nusu za kitanzania, pia alinunua nyumba nyingine kwa  £ 311,000 (UK), pia kanunua mansion South Africa kwa £3.2Million, Magari kadhaa aina ya Range Rovers kwa £600,000, Gari aina ya Bentley £120,000, Mercedes Maybach kwa Euro 407,000.


Kweli Africa raha huyu ni kiongozi mmoja tu!! Je serikali zetu zina pesa kiasi gani? (TAFAKARI......!!!!!)


Kwa habari zaidi soma HAPA