12 August, 2011

...............NEW GADDAFI IN TOWN!!!!!!




Gaddafi Chameleone (LOL)
Msanii nguli wa miondoko ya ragga  nchini Uganda bwana  Joseph Mayanja aka Jose Chameleon ambaye pia anajiita dactari wa muziki abadili dini yake Catholic na kua Muislam.Mwanamziki huyu ambaye miaka michache iliyopita alioa na kufunga harusi katika dini ya kikristo na hata kuokoka (SOMA HAPA) amewaacha watu wengi midomo wazi baada ya uamuzi wake huo wa ghafla.
                                    Gaddafi Chameleone akifuatilia maelezo
Leo Ijumaa ya tarehe 12/08/2011 Chameleone ambaye jina lake kwasasa ni Gaddafi Chameleon ameonekana msikiti wa Kibuli akihudhuria swala ya Ijumaa.Hivi Gaddafi ni jina la kiislam?? Anayejua atujulishe!


Zaidi soma HAPA

KWELI USWAHILINI KUNA VITUKO!!!

Dakika ya  0:59
                 1:07
                 1:32
                 2:23
                 3:50

PICHA ZA MATUKIO MBALIMBALI VURUGU ZA UK

 Picha mbili za mwanzoni hapa chini waandishi wa habari wamezipa majina ya pekee kabisa kutokana na matangazo ya biashara nyingi hapa UK. Mfano ''Buy now pay later'' yaani nunua sasa ulipe siku nyingine.Aidha katika vurugu zinazo onyesha kupoa zoezi hilo la kuiba vitu limepewa jina la ''Take now don't pay later'' Yaani chukua sasa na usilipe baadae!.Waziri mkuu David Cameron amesema kila aliyehusika na vurugu,wizi na uharibifu ajue watamfikia na atawajibishwa!
Usemi huo hapo juu naufananisha na ule wimbo wa Twanga 'mtaji wa masikini nguvu zake mwenyewe' ambao majambazi  bongo waliwaimbisha abiria wa mabasi/magari yaliyo tekwa huku wakisachiwa walivyo navyo.
   


                                   Magari yaliyo chomwa moto Serikali imeahidi kulipa fidia

                                Duka likiwa limevunjwa kioo,wenye maduka pia watalipwa fidia

                               Aidha uruke toka juu gorofani au ufe kwa moto dada aliona kuruka ni bora
                       
                               Polisi wakiwa wanaangalia kinacho endelea na wananchi wenye hasira kali
 Jamaa wakiwa tayari kwa vurugu na kubeba kinacho bebeka.Kama unavyowanona wameficha sura nchi hii ni moja wapo ya nchi zenye CCTV camera nyingi duniani kwahi ukifanya kosa ni rahisi kukukamata.Lakini hapo CCTV haina ujanja!


Baba wa kijana miongoni mwa wale vijana watatu waliouwawa katika vurugu jijini Birmingham akiongea kwa uchungu kufuatia kifo cha mwanae ambaye inasemekana alikua akiokoa majirani waliokua wamevamiwa katika vurugu hizo hadi mauti yalimpomfika.


Kwa habari zaidi BOFYA HAPA