14 September, 2011

MABADIRIKO TAREHE YA HARAMBEE KUCHANGIA MAAFA ZANZIBAR KWA WATANZANIA UK


Kutokana na sababu zisizoweza kuzuilika Jumuiya ya Watanzania nchini Uingereza TANZ- UK  inawaomba radhi wanajumuiya na watanzania wote kuwa shughuli za fund-RaƬsing zilizokuwa  zifanyike katika ubalozi wetu london siku ya jumamosi tarehe 17 septemba 2011 saa nane mchana zimeahirishwa. 

Taarifa zaidi zitawafikia hapo baadaye, tutawajulisha punde tu tutakapo pata habari kamili. Tafadhali mjulishe na mwenzako

ASANTENI
 MWENYEKITI, 
TANZ-UK

MIDA YA KAZI- DULLAYO (VIDEO)


13 September, 2011

VITUKO AJALI YA MELI ZANZIBAR

ati mMILIKI WA MV SPICE ISLANDERS HAJULIKANI!!.HII HAIINGII AKILINI HIVI KWELI CHOMBO KIKUBWA KAMA HIKI KILIKUA KINAFANYA BIASHARA NA MMILIKI HAJULIKANI HII INA MAANA GANI?.NDIO TUSEME NDIO MFANO WA BIASHARA BUBU ?.NINA IMANI KAMA KIMEKUA KIMESHINDA TUZO ZA KAZI NZURI BASI MMILIKI ANGEJITOKEZA HARAKA LAKINI KWAKUA KIMELETA AIBU KWA TAIFA NDIO MMLIKI HAJULIKANI.MAMLAKA HUSIKA ZITAWAAMBIA NINI WATANZANIA AMBAO WAMEPOTEZA NDUGU ZAO KWA UZEMBE.JE MV BUKOBA HAIKUTOA FUNZO? JE WAKATI INAONDOKA BANDARINI HAIKUKAGULIWA KAMA INA MZIGO UNAO STAHILI TUKIACHIA MBALI UCHAKAVU WAKE? JE HII NI MOJA YA BIASHARA KUBWA AMBAZO HAZILIPIWI KODI? HAPA SERIKALI ISIPO WAJIBISHA WAHUSIKA BASI NI WAZI WATANZANIA WATAJUA KUNA MWANYA WA RUSHWA WA WAZIWAZI.NA KAMA HII HABARI HAPA CHINI NI KWELI BASI NI AIBU KUBWA!!


                                      >>>>>> SOMA ZAIDI HAPA CHINI NI AJABU>>>>>
BY DR. WOLFGANG H. THOME, ETN UGANDA | SEP 12, 2011
(eTN) - In an extraordinary, though not unprecedented turn of events, the government of Zanzibar has reportedly denied having any knowledge of the registered owners of the MV Spice Islander. The Spice Islander is the ferry between Unguja - commonly referred to as Zanzibar - and Pemba, that capsized and sunk on September 10, 2011 with over 600 or 800 people on board - the number has yet to be determined - leaving scores of passengers dead in the water and others struggling to survive by clinging on to debris until they could be pulled out of the water by rescuers.
Registration and licensing of ocean going vessels, however, has been confirmed to be a function of government by tourism stakeholders, one of whom said this in an email overnight:
"This is not just unreal but almost mocking those seeking answers, those who lost relatives on the islands. How can a government claim not to be aware of the owners and it is the same government giving them a license.
"We are also disturbed about conflicting figures, some of which put the total passengers to over 800 and then government mouthpieces try to shrink these figures to within the licensed number. What is going on here?
"The tragedy was avoidable if only rules were enforced. There is notorious corruption across all outlets of public services, and they are now just trying to whitewash the whole thing.
"It is high time that government brings us new safe ferries, which can be used to travel from one island to the other without risking our lives every time one sets foot on board."
The central government in Dar es Salaam did, according to media reports, release 300 million Tanzania Ssillings to assist bereaved families with funeral expenses.
The official number of casualties was given by a Zanzibar government spokesperson as just under 200 with nearly 600 survivors, which would put the overall number of passengers on board well over the licensed figure permitted. There is also no certainty over the number of bodies not yet recovered, as apparently no complete passenger manifest was produced prior to the ferry leaving for its last ill-fated journey to Pemba.
Reconciling survivors and casualties is, therefore, literally impossible for the authorities in Zanzibar. It is understood that Kenyan authorities are now also keeping a watch along the shores from across the Pemba Channel, in case any bodies would be spotted across the international border.
A legal aid organization is planning to sue Zanzibar's government and others involved for negligence. For more READ

HARAMBEE NCHINI UINGEREZA KUCHANGIA WAHANGA WA AJALI YA MELI ZANZIBAR




Jumuiya ya waTanzania nchini Uingereza TANZ-UK ikishirikiana na Jumuiya ya Wanzanzibar waishio Uingereza (ZAWA), Urban Pulse na Miss Jestina George Blog imeandaa harambee (fundrising) maalum kwa ajili ya kuweza kuwasaidia waathirika wa ajali ya meli ya Spice Islander iliyotokea Nungwi njiani kuelekea Pemba. Fundrising hii itafanyika katika Ubalozi wetu hapa London tarehe 17 Septemba 2011 Kuanzia saa nane mchana.


Tunawaomba Watanzania wote mlioko hapa nchini Uingereza kutoka jumuiya mbalimbali,vyama vya kisiasa, wafanyabiashara, wanafunzi na hata wasio Watanzania mjitokeze kwa wingi ili kuweza kujumuika nasi na kufanikisha zoezi hili. Hivyo basi tunaomba mwenye fedha au chochote kile cha kuweza kuthamanishwa tunaomba tuweze kuja nacho na kitafanyiwa mnada. Mfano, wenye biashara wanaweza wakaleta bidhaa kiasi ambazo zitafanyiwa mnada ambapo ziada itakayopatikana itakuwa sehemu ya mfuko tutakaokuwa tunautafuta.

anwani ni; 3 Stratford Place, London, W1C 1AS. Muda ni saa nane mchana (2pm sharp).

Kwa maelezo zaidi tunaomba uwasiline na:-
Mwenyekiti Tanz-UK 07766856565,
ZAWA 07538063536,
TA London 07404332910

UKIONA TANGAZO HILI TAFADHALI MTAARIFU NA MWENZAKO. WOTE TUNAKARIBISHWA,Mungu ibariki Zanzibar, Mungu ibariki Tanzania, Mungu ibariki Africa . Zaidi sana Mungu wabariki Watanzania wote popote pale walipo duniani.
ASANTENI.
MWENYEKITI,
TANZ-UK

POLENI WAFIWA NA MAJERUHI AJALI YA MELI ZANZIBAR


                                        10/09/2011
Kweli ni pigo kubwa kwa mara nyingine Taifa lapoteza ndugu zetu katika ajali ya meli Zanzibar.Pole nyingi ziwafikie ndugu, jamaa na marafiki kwa kuondokewa na wapendwa wao.
Poleni sana ndugu zetu   na tusichoke kumuomba Mungu atujalie hekima na uvumilivu katika kipindi hiki kigumu pia awajalie viongozi wetu hekima zaidi waweze kukwepa majanga yaliyo ndani ya uwezo.  

Mwenyezi mungu azipumzishe roho za marehemu mahali pema peponi na kuwaponya haraka walio nusurika. AMEN

Zaidi soma HAPAHAPA & HAPA

08 September, 2011

ANASEMA MUACHE KUMCHAFUA!!!

Bila shaka ujumbe umefika japo lugha aliyotumia hajaitendea haki kwa Tanzania ninayo ijua, kuna Holly fu*k na f*ck & Sh*t. Sijajua ilikua hasira au njia mpya ya kufikisha ujumbe! Kikawaida hayo maneno ni makali ukizingatia hii video imekusudiwa kuwekwa hadharani via youtube. Well, is freedom of speech/expression  lakini ujumbe ungefika vizuri kwa lugha nzuri na sio matusi.NI MTAZAMO TU WA KIBARAZA HIKI   KWA DADA YETU NA PIA IWE CHANGAMOTO KWA CELEBS WENGINE MNAPO AMUA KUONGEA YANAYO WAHUSU!

HII BADO NI CHANGAMOTO KUBWA KWA SERIKALI

Mkuu wa mkoa wa Rukwa Daniel Ole Njoolay akikabidhi ambulansi ya "kisasa" aina ya bajaj kwa mkuu wa wilaya ya Mpanda, Dk Rajab Rutengwe (kushoto). Ambulansi za miguu mitatu zimesambazwa na serikali kusaidia kutoa huduma za afya vijijini ambapo mkoa wa Rukwa utapokea miguu hii mitatu 20. Picha na Hamza Temba!!! 

Maswali:
>>Je huyo mgonjwa atapataje huduma ya kwanza?
>>Je dereva atakua daktari/muuguzi ama?
>>Je kwa barabara tulizo nazo hii miguu mitatu  inakidhi kiwango?

Maoni:

>>Serikali tunashukuru kwa kutoa huduma ambayo ni tatizo sehemu nyingi Tanzania lakini hii haikidhi mahitaji kwa karne hii ya 21 bila kusahau miundombinu yetu ambayo bado sio mizuri sehemu nyingi.

>>Ni bora zinunuliwe gari hata za kawaida (kama lengo ni kubana matumizi of which sina hakika kama hizo bajaji ni bei ndogo!) japo kufikisha mgonjwa hospitali ila sio pikipiki kwani ni rahisi mgonjwa kudhurika na jua,mvua (utelezi wa barabara kipindi cha masika), vumbi,au hata ajali kwani ni rahisi kupata ajali kwa pikipiki kuliko gari.

>>Kununua pikipiki kama nyenzo ya kusafirishia wagonjwa wakati wewe unatembelea  Landcruiser V8 (4.7Litre posh and expensive) hakuleti picha nzuri kwa wapiga kura na walipa kodi kwa ujumla au kwa maneno mengine serikali haijali wananchi ambao wameipa ridhaa ya kuwatumikia kwani hata 
matunda ya kodi zao hayaridhishi!


Free Thinking aka Mpayukaji  naye katoa  maoni yake kuhusiana na changamoto hii yasome  HAPA

TMK CHEGGE & TEMBA NDANI YA COVENTRY KESHO IJUMAA

Ijumaa hii ya tarehe 09/09/2011  wapenzi wa TMK watakua wanapata burudani ya nguvu toka kwa Chegge
 & Temba hapa |Coventry.Wale tusio penda stress basi tukanyooshe mkono mmoja juu pale PALMS BAR, Address ni 116 FAR GOSFORD CV1 5EA.Tuonane huko!!

                          Tukaweke mkono mmoja kama hivi!!

07 September, 2011

RAFIKI ZANGU WAKUMBANA NA FRAUD!!!!

Wanasema kuuliza sio ujinga na ni kweli rafiki zangu wawili wakumbana na michezo ya wizi mitandaoni lakini wakaamua kuuliza baada ya kupata wasiwasi na kushinda pound kibao na wakati huo huo kutakiwa kutoa kiasi kidogo cha pesa ili wapewe pesa wanazo dai wameshinda.Sasa mie najuuliza kama nimeshinda kweli si wapunguze zile ambazo nimeshinda na zilizo baki wanipe kwanini wanataka niongeze pesa? well tujiunge na kisa hapa chini


Mdau  wa kwanza:
 To: rijaki@ymail.com
Sent: Sunday, 4 September 2011, 14:51

Leo nimepata email toka huko uingereza kwa mtu aliyejitambulisha kama Angelina Keith mwenye umri wa miaka 87 ambaye mumewe alikufa kwenye ajali ya ndege. Kwa kuwa walikuwa na uwezo sana basi sasa anadai ameamua kuishi katika ranch yao na karibu asilimia 30 ya mali zake amegawia charity mbalimbali na kiasi kingine ameandikia check kwangu na kuiacha DHL london kwa lengo la kutuma huku. katoa jina, namba ya simu na namba ya siri ya bahasha (brown envelope) yenye hiyo check nikatuma email kwa hao DHL wakasema ni kweli kuna hiyo bahasha ninachotakiwa ni kupeleka taarifa zangu kama jina, anuani namba siri na kisha nitatakiwa kulipia security fee pound 160 kisha wataleta.


 Nimeona kama vile hata wazungu wanaweza kuwa matapeli hebu niambie aina hii ya wizi ipoje hapo Uingereza. maana nimepiga simu yamepokea na kufuatilia kisha yakajibu lakini nimeona haiji akilini.....................Nikamshauri aachane mara moja na hao wezi mitandaoni kama haitoshi mdau huyu akataka kujua zaidi kwa kufuatilia DHL ndipo akabaini mchezo huo wa wizi na akanijibu......


Tuesday, 6 September 2011, 10:01


>>>kweli bwana majamaa haya ni majizi inavyonesha maana yanajifanya yanafanya kazi DHL Express lakini nimefungua mtandao wa DHL sijaona namba za simu yenyewe yanapiga simu karibu kila siku kuulizia nimelipa na kama nimelipa ni scan risiti ya malipo nitume kwa mtandao haraka.


Mdau wa pili:
Huyu alianza na kuulizasorry,eti unafahamu mashindano ya iphone mobile promo,mama yangu katumiwa meseji ya kushinda unaweza kunichunguzia maana isije ikawa matapeli,naomba 
uniulizie,kama ni kweli


*Nikaomba kupata maelezo aliyopata kwenye ujumbe nayo ni:-


message imetoka iphone mobile promo UK, iliandikwa kuwa your cell phone number has won 715000 pounds from I- PHONE-UK,for claims of prize wakatutumia email iphoneclaims @gmail.com.ss tulivyo watumia meseji ya kupata huo ushindi waka tutumia verification form ambayo tulijaza jina la mama,namba ya cm ya ushindi anuani,network name ,maana wanasema ni mashindano ya kwanza yaliyo tumia automated ramdom computer kwa kutumia namba za simu,sasa walipotoa option ya kupata pesa kuna ya kufuata huko london hadi adress wametoa,au njia ya ndege ambayo ni cheki au kutumia bank ya western union .sisi tuliomba watumie njia ya barclays ,wametutumia form ya barclays lkn ukitumia njia hiyo wanatuma kama dollars.na mtu ambaye amepewa jukumu hilo ni stephen elop na namba za simu wametoa ambazo ni+4915118186861
naomba unitafitie maana wametoa hadi Adress zao za hapo london na iko under BRITISH LAW.



**Ndugu wasomaji hizi ni fraud (kudanganya ili kupata pesa) na nime post nyingi sana katika blog hii.Wanaweza kukupata kwa njia ya simu,email au hata barua kwa njia ya posta kwa hio ukipata ujumbe kama huo si vibaya kuuliza au kuupotezea ukifanya kimya kimya basi jiandae kulia kilio cha samaki!!.Dar es salaam na sehemu nyingine watu wameibiwa eti mtu anakuambia ananunua paka mweusi kwa MILLION 2 hivi mtu huwezi shituka kama ni wizi unataka kufanyika?.Kiufupi nimefurahishwa na hawa ambao wameuliza na nimesha wajibu huu ni wizi tu wa mitandaoni waachane nao**


Kwa habari zaidi kuhusu fraud bonyeza HAPAHAPAHAPA HAPA NA HAPA  











05 September, 2011

NI AJABU LAKINI KWELI.. MAHUBIRI YA KUIKATAA CCM

HUYU PASTOR/MCHUNGAJI KATOA MAANA YA CCM KAMA CHAMA CHA MAJAMBAZI, KAMA HAITOSHI AZIDI KUKIBOMOA CHAMA HICHO KWA KUSEMA MUNGU HATAKI CCM,SWALI JE ANAPENDA CHADEMA,NCCR AU CUF??.SIKUMBUKI KUSOMA SEHEMU INAYOSEMA KANISANI/MSIKITINI WATU WANAENDA KUJIFUNZA SIASA ZAIDI YA KUFANYA IBADA AU KUSWALI!!


JE WEWE HUA UNAENDA KANISANI/MSIKITINI KUFANYA NINI??
HUYU KWA MTAZAMO TU HANA TOFAUTI NA HUYU
NA KWA HAKIKA ANGEKUA CCM NI HUYU HUYU ANGETUAMBIA MUNGU ANAPENDA CCM.UKISIKILIZA DAKIKA YA 1:37 ANASEMA ''Slaa iko mikononi mwako itumie vizuri kura yako'' MPAKA HAPO MPENZI MSOMAJI UTAJUA YEYE CHAMA GANI NA BILA SHAKA HICHO NDIO ATASEMA  MUNGU ANAKIPENDA!!

TOYOTA LANDCRUISER VX YA 2011

Kampuni ya Toyota inazidi kuwafurahisha wateja wake kwa kuzidi kutoa gari nzuri 4x4 kama Landcruiser VX Toyota Rav4 na nyingine nyingi.Kwakua hii ndio kazi yangu usisite kuniagiza nikutafutie gari (kwa anaye taka gari toka UK aina yoyote mfano Jaguar,Toyota,Range Rover,Suzuki,Scania, Mercedes Benz,BMW n.k)  kama nilivyosema kwenye blog hapo juu sambamba na 'dhumuni la blog' nimeona si vibaya kwa leo nilete japo picha za Landcruiser VX ya 2011 na ili uone muonekano wake na narudia tena ukitaka gari kutoka UK nipigie +447552621975 au niandikie via rijaki@ymail.com.Mwisho niseme asante kwa mlio toa ushirikiano tayari kupitia blog hii.


                  Mwonekano wa ndani sehemu ya mbele kwa dereva na dashboard



                                            Kwa nje upande wa ubavu wa kushoto na nyuma
   Kwa mbele na ubavu upande wa kulia kwa dereva

ETI 'VAT' MAANA YAKE VATICAN?????

Kipande hiki cha video kimeeleza mambo kadha wa kadha yenye wasiwasi kama sio upotoshaji eti VAT ambayo ni 'Value Added Tax (Kodi ya Ongezeko la thamani) kama 'Vatican' na watu wanaitikia? Mwl.Nyerere apondwa eti alikua kiungo muhimu wa makanisa na alifanya maisha kuwa magumu na mzee Ali H Mwinyi maarufu kama Mzee Ruksa afagiliwa.Sambamba na hayo Chama Cha Mapinduzi (CCM) kimedaiwa kuwa ni chama cha makafiri na kama yeyote aliye serikalini au CCM ngazi yeyote ana swali basi huyu jamaa yupo tayari kujibu.Aidha kanisa katoliki limetajwa kubomoa uislam(udini wa nini Tanzania?)

Kwa mengine mengi sikiliza hii clip ni ajabu na nimeshindwa kushangaa labda sijaelewa sikiliza na wewe mpenzi msomaji wa kibaraza hiki




30 August, 2011

EID MUBARAK WADAU WOTE POPOTE MLIPO



SINA MENGI KWA LEO NIWATAKIE TU EID NJEMA MSHEREKEE KWA UPENDO NA AMANI,MSISAHAU KUOMBEA WAGONJWA, KUSAIDIA WENYE SHIDA,MASIKINI,YATIMA WENYE NJAA N.K.KIBARAZA HIKI KINAWATAKIA KUSHEREKEA VYEMA MWISHO WA MWEZI MTUKUFU WA RAMADHAN

29 August, 2011

MAANA HALISI YA VIJISENTI HII HAPA

Kama hii ni kweli basi mtu yeyote ambaye amewahi sikia kuhusu ''vijisenti'' angekubali kua kauli hio ilikuwa na ukweli ndani yake!!Kwa habari zaidi kuhusu vijisenti SOMA HAPA.

21 August, 2011

KUTOKA LIBYA:WAASI WAINGIA MJI MKUU TRIPOLI

Habari zilizojiri kutoka Libya zinasema mapigano makali yatikisa mji mkuu Tripoli kati ya waasi na wanajeshi wa serikali nchini humo.Watu zaidi ya 1000 wadaiwa kufa na wengine 5000 kuumia vibaya.Katika mapigano hayo makali yaliyozuka mida ya saa asubuhi leo waasi nchini Libya wamedai kumteka mtoto wa Gaddafi Saif Al-Islam. Kwa habari zaidi soma HAPA

19 August, 2011

HABARI NJEMA ZA SCHOLARSHIP UGHAIBUNI

Kama ilivyo ada kutoa habari mbalimbali zinazo husu scholarship leo nimeona nilete link ambazo zinaendana na mambo kama hayo.Zisome hizo link kwani nina imani zitakua na msaada kwa namna moja ama nyingine iwe kwako,nduguyo au rafiki yako.Hata hivyo ukipata habari kama hii si vibaya kumpa na mwenzio hivyo ndivyo tunaweza sambaza taarifa hii mpaka kwa wahitaji.


Soma hii kuhusu scholarship kupitia Michuzi blog kwa KUBOFYA HAPA
Pata habari za scholarship kwa kujiunga mjadala kwa KUBOFYA HAPA
Habari muhimu za scholarship bonyeza HAPA na HAPA
Soma zaidi habari  za scholarship   HAPA
Kuwa makini na utapeli wa scholarship  SOMA HAPA

17 August, 2011

SCHOLARSHIP KWA WATANZANIA SHEFFIELD UNIVERSITY-UK


Wadau mnaotafuta scholarship nimepita  The habari leo ambao unaweza kuwasoma HAPA kwamba chuo cha Sheffield kinatoa Scholarship kwa wanafunzi wa Kitanzania walioonyesha uhodari mkubwa katika masomo yao, na wana dhamiria kujiunga na Chuo hicho Septemba, 2011. Kwahio changamkieni hio muda ndio huo ushayoyoma
Ukitaka  maelezo zaidi, fika ofisi za wawakilishi wa Chuo hicho waliopo Tanzania kwa anuani ifuatayo:
Wawakilishi Tanzania

Wawakilishi maalum wa Chuo cha Sheffield Tanzania ni:

Uniserv Tanzania
Haidery Plaza, 1st Floor
A. H. Mwinyi Road/Kisutu Street.
Dar es Salaam, Tanzania
Tel: +255 0(22) 2129036
Mobile: +255 787 019037 or +255 787 019047.
Fax: +255 0(22) 2129037
Kwa habari zaidi  toka chuo cha Sheffield wenyewe BONYEZA HAPA
Aidha kujua zaidi kuhusu scholarship za Uingereza na maisha  kwa ujumla tembelea British Council  kwa ku  BONYEZA HAPA 

Au wasiliana nao kwa anuani ifuatayo.
Samora Avenue / Ohio Street
P.O BOX 9100
Dar es Salaam,Tanzania
Simu:+255 (0) 22 2165300
Fax:  +255 (0) 22 2112669/2116577

 


16 August, 2011

TUNES OF THE WEEK (BONGO FLAVA)

Hii leo ndio list yangu ya Miziki mizuri ya Tanzania (Bongo flava) ikiongozwa na AY ft Lil Romeo,Lamyia.Hizi ni baadhi ya nyimbo bora za wasanii wetu siunajua mcheza kwao hutuzwa basi unaweza sikiliza kwa kubonyeza moja baada ya nyingine .Raha jipe mwenyewe usisubiri kupewa.




HIVI KWELI MAPENZI SUMU?

Kwa wale ambao wamekwisha chukua maamuzi magumu ya kuoa hasa miaka yasasa wanaweza kua na majibu  sahihi ya hili swali.Lakini pia katika harusi zote nilizo hudhuria hua sikosi kusikia ''MKAVUMILIANE NA KUHESHIMIANA'' hivi vitu viwili vikikosekana lazima ndoa iyumbe kwa namna moja ama nyingine.Hata hivyo ndoa sasa hivi hazidumu je tukubali kua mapenzi ni sumu?.Kimtazamo kama usemi huu una ukweli  kwa asilimia kubwa basi ishakua balaa!!

Mie nilikua nadhani ukiwa na mpenzi (Mke/Mme) basi ni raha kumbe inaweza kua kinyume chake.Na kwakua sasahivi ndio wanaita muda wa haki sawa,kwenda na wakati basi talaka ndio nje nje tujiulize kwanini?.Mbali na hio vijana sasahivi wanachelewa kuoa/kuolewa je tatizo ni nini?? Wengine wanasema ndoa ndoano je hii ni sababu ya ambao hawajaoa kutooa mapema?

Mtazamo wangu, kwakua imekua mila na desturi sehemu nyingi Africa hususani Tanzania toka zamani tumeona mwanaume ndio mtoa maumuzi ya mwisho (aka kichwa cha familia) si vibaya kwasasa mwanamke kushirikishwa katika maumuzi mbalimbali katika familia.Kusingizia haki sawa miongoni mwa wanawake na kujenga kiburi mwisho wake talaka.


Ni lazima kuheshimiana na kusikilizana kwa wapenzi/wanandoa (kama mnataka kufurahia).Mambo uliyofanya ukiwa pekee yako lazima uangalie kama yana mchango mzuri katika mahusiano kama sivyo basi achana nayo.Imekua utaratibu sasa hivi wapenzi kusema wanataka uhuru unakuta mtu kaoa/kaolewa na bado ana mawasiliano ya karibu na mpenzi wa zamani ya nini hasa?


 Hii tabia sio nzuri ndo mwanzo wa kupokelea simu chooni,kuzima simu ukiwa na wako,kuweka silent na kuwekeana password ambazo huongeza maswali ni je unaficha nini?? Mambo ya vidumu mpaka lini na magonjwa yaliyozagaa?? Nadhani hii ni moja ya sumu ya mapenzi, na kwanini tusiite mapenzi raha/matamu na maneno kama hayo kwa kuepuka hizo sumu ambazo ziko wazi?

MUWEKEZAJI AKIONA MANENO HAYA LAZIMA AKIMBIE SANA.


Au wewe unaonaje? Hii kwa muwekezaji haina maana tofauti na ile ya mzazi (anaye penda mtoto afauru) kupeleka mtoto wake shule ambayo anaambiwa haina walimu,vifaa vya kufundishia,mtoto atakaa chini (hakuna viti vya kutosha) wakati anasoma,hakuna vitabu,maktaba n.k huyu atakua mzazi wa ajabu katika dunia hii.Sasa tujiulize ni muwekezaji  gani toka ndani/nje atatamani kuwekeza nchi haina umeme,maji na mafuta??.
Kipengele cha hakuna serikali (No Government) siamini labda tuseme haijawajibika katika baadhi ya mambo.

13 August, 2011

KUCHEKA NI.....................................???

Matatizo ya umeme na Orijino komedi
                                     

                             Matumizi ya Lugha....kisa cha chips zege (LOL)

12 August, 2011

...............NEW GADDAFI IN TOWN!!!!!!




Gaddafi Chameleone (LOL)
Msanii nguli wa miondoko ya ragga  nchini Uganda bwana  Joseph Mayanja aka Jose Chameleon ambaye pia anajiita dactari wa muziki abadili dini yake Catholic na kua Muislam.Mwanamziki huyu ambaye miaka michache iliyopita alioa na kufunga harusi katika dini ya kikristo na hata kuokoka (SOMA HAPA) amewaacha watu wengi midomo wazi baada ya uamuzi wake huo wa ghafla.
                                    Gaddafi Chameleone akifuatilia maelezo
Leo Ijumaa ya tarehe 12/08/2011 Chameleone ambaye jina lake kwasasa ni Gaddafi Chameleon ameonekana msikiti wa Kibuli akihudhuria swala ya Ijumaa.Hivi Gaddafi ni jina la kiislam?? Anayejua atujulishe!


Zaidi soma HAPA

KWELI USWAHILINI KUNA VITUKO!!!

Dakika ya  0:59
                 1:07
                 1:32
                 2:23
                 3:50

PICHA ZA MATUKIO MBALIMBALI VURUGU ZA UK

 Picha mbili za mwanzoni hapa chini waandishi wa habari wamezipa majina ya pekee kabisa kutokana na matangazo ya biashara nyingi hapa UK. Mfano ''Buy now pay later'' yaani nunua sasa ulipe siku nyingine.Aidha katika vurugu zinazo onyesha kupoa zoezi hilo la kuiba vitu limepewa jina la ''Take now don't pay later'' Yaani chukua sasa na usilipe baadae!.Waziri mkuu David Cameron amesema kila aliyehusika na vurugu,wizi na uharibifu ajue watamfikia na atawajibishwa!
Usemi huo hapo juu naufananisha na ule wimbo wa Twanga 'mtaji wa masikini nguvu zake mwenyewe' ambao majambazi  bongo waliwaimbisha abiria wa mabasi/magari yaliyo tekwa huku wakisachiwa walivyo navyo.
   


                                   Magari yaliyo chomwa moto Serikali imeahidi kulipa fidia

                                Duka likiwa limevunjwa kioo,wenye maduka pia watalipwa fidia

                               Aidha uruke toka juu gorofani au ufe kwa moto dada aliona kuruka ni bora
                       
                               Polisi wakiwa wanaangalia kinacho endelea na wananchi wenye hasira kali
 Jamaa wakiwa tayari kwa vurugu na kubeba kinacho bebeka.Kama unavyowanona wameficha sura nchi hii ni moja wapo ya nchi zenye CCTV camera nyingi duniani kwahi ukifanya kosa ni rahisi kukukamata.Lakini hapo CCTV haina ujanja!


Baba wa kijana miongoni mwa wale vijana watatu waliouwawa katika vurugu jijini Birmingham akiongea kwa uchungu kufuatia kifo cha mwanae ambaye inasemekana alikua akiokoa majirani waliokua wamevamiwa katika vurugu hizo hadi mauti yalimpomfika.


Kwa habari zaidi BOFYA HAPA

11 August, 2011

UKISIKILZA WIMBO PEKE YAKE UTADHANI CHAMELOENE


Fanya kazi
                                                                    Sweet mama

TANZANIA BILA UMEME/MAFUTA INAWEZEKANA??

Ilikua.........................

Heshima ikajengeka mjini na salamu zikatolewa kama hivi.........

Ghafla bin vuuu mara...........
Vidumu ndio mpango duh kweli Bongo Raha! hapo bado adha ya umeme,maji safi,foleni,stress binafsi n.k

Wauza wese nao wataka heshima!! sijui wanataka salamu kama hio ya Tanesco?.Hakika hivyo vituo vya mafuta  vingekua tu huku kwenye vurugu zilizo anza baada ya mtu mmoja tu kuuawa basi zingebaki historia,magofu ama kuchukuliwa mafuta yao kwa nguvu tena bure 'yaani take now don't pay later' kama ambavyo tutaona matukio zaidi yaliyo jiri hapa UK.Watu wamechoka na blah blah wakati maisha magumu.Siombei tufikie huko lakini huenda ndiko tunako elekea bila kujijua. Je viongozi wetu wanaliona hili? au wao haiwahusu? Nauliza tu!