Showing posts with label Katuni ya Leo. Show all posts
Showing posts with label Katuni ya Leo. Show all posts

04 August, 2011

TUSIFIKIE TU HATUA HII .....ha ha haa !!!

Kufuatia sakata la kufukuzwa wabunge  toka mjengoni katuni hapa chini imenifurahisha sana kwa namna ujumbe ulivyofikishwa.Sasa tukifikia hatua kama hii sipati picha Bunge litakuwaje.Nadhani mchora katuni  ameonyesha  dawa ya uonevu ipo jikoni ipo siku utapatiwa suluhu ya namna hio ama inayoendana ili kwenda sawa ama kukomesha hali hio kabisa.Tujiunge ha ha haaaa!!! yani sina mbavu.Hongera Abdul




                                      Kesho kutwa!!!!?

Sasa hii ya hapa chini sijui wanamfurahisha nani? Kama bajeti haifai kwanini uipitishe? Huyu ndio mwakilishi wa mpiga kura!! Je tuseme wabunge wa namna hii hawajui majukumu yao bungeni?? Nadhani wabunge wa namna hii ndio wafukuzwe bungeni hawana faida na mwisho wataishia kulala tu wakati mjadala ukiendelea!
                          Kuna mwenye majibu swali ndio hilo, sema usikike!

27 June, 2011

LIBRARY...

Kwa wale wapenda kusoma vitabu hasa unaposomea maktaba haya mambo yapo sana (angalia picha hapo chini).Hata madarasani kuna wadada wanaova nguo ambazo ukikaa kiti cha nyuma yake unaona shanga,nguo ya ndani n.k.Mie hua najiuliza kama msomi ana vaa vile tena akiwa katika mazingira ya kusoma huko mtaani ana vaa vipi na je jamii inamchukuliaje? Je ndio kuishi kisasa au kishamba? Kwani ukijisitiri vizuri unapungukiwa na nini?






Kwa walio soma UDSM pale chini ya mti wanaita mdegree haya mambo ndio usiseme sijui kama kuna mtu anasomea pale anaelewa! labda kipindi cha mitihani ambapo unaweza somea sehemu yenye kelele za kutosha na ukaelewa kama kawaida.Kama mdegree bado ipo mtazamo wangu naona inafaa kwa mijadala ya vikundi ama kupumzika baada au kabla ya kipindi. Mwisho kabisa ushauri wa bure kwa dada zetu vyuoni na popote pale wapatapo ujumbe huu wavae vizuri kusitiri miili yao wengine inakua vigumu kuvumilia unapo ona maungo ya kike na wakati mwingine kama unasoma unaweza shindwa kuelewa unachosoma

14 June, 2011

MAMBO YA MPANGALA!!!!

                                    Chanzo:komic first

Tuseme ukweli ukiachana  na hii ya Mpangala kama hali iko hivi Bungeni basi hio posho iondolewe maana sio haki kama mtu unalala  fofo bungeni hio michango ya maendeleo ya jimbo lako unatoa wapi na saa ngapi? Yaani kulala ulale na ukiamka ulipwe?  Angali huyu!! sasa akiamka hapo ni  kugonga meza hoja imepita hata kama hajui inahusu nini (hapa ndipo ninapo wapendea wapiga picha)




Kwa katuni zaidi SOMA HAPA

24 August, 2010

Katuni ya leo

Hapa nani kashinda wadau hahahaha! Kama mambo yenyewe ndio haya gonjwa la UKIMWI tunalikaribisha nyumbani kwetu kwa nguvu zote na mwisho wa siku tuanze kuulizana nani kauleta.Ungejibu nini kama swali kama hilo linakutokea??