09 August, 2010

Polisi UK wala bata kazini

Hapa UK polisi wa usalama barabarani hawajua kuchomwa na jua ni kitu gani kwani imekua tofauti kabisa na Tanzania ama nchi nyingi zinazo endelea ikiwemo Africa.Wenyewe vidhibiti mwendo ni kama inavyo onekana kwenye picha hapo chini.Ukitembea mwendo usio ruhusiwa basi risiti ya fine utatumiwa nyumbani kwani hio camera inapiga picha gari zote zinazo tembea kwa speed hatarishi/isio ruhusiwa kuanzia motor ways mpaka barabara za kawaida.Kwa maana hio hakuna haja traffic kujificha porini na camera kwani wanaweza hata liwa na simba (L0l-joke)

Mbali na hivyo vitendea kazi walivyo navyo mfano magari ni dalili tosha kwamba serikali yao iko makini katika ulinzi na usalama kwani magari wanayo ya uhakika mfano BMW X5, D529, Range Rover, Hummer,lambourgini, Lotus, Lexus,Jaguar,Ford,Astra, Landrover Deffender, Mecerdes Benz na nyingine nyingi bila kusahau helicopter ambazo zina nembo ya polisi na nyingine hazina ukitaka kuona picha zaidi ingia hapa http://www.google.co.uk/images?hl=en&source=imghp&biw=1276&bih=605&q=police+cars+UK&gbv=2&aq=f&aqi=g1&aql=&oq=&gs_rfai=
Pia kujua kama gari lako lipo barabarani kimakosa mfano kutokua na insurance, gari la wizi n.k sio lazima polisi akusimamishe akiwa kwenye gari lake either mbele au nyuma yako basi anaweza jua gari lako lina makosa na ukasimamishwa kwa mahojiano zaidi.


(camera ya kudhibiti mwendo na uhalifu barabarani-UK )


Aidha polisi ni washikaji/rafiki wa kila mtu na hawaogopwi kama wetu huko Africa, hawa wa huku UK unaweza hata ukaomba hata lift hawana noma provided makaratasi yako yapo valid maana unaweza kua kama panya alie ingia zizi la paka bila kujali litakalo tokea. Pia ukienda club wanakuwepo wengi tu nje pamoja na Ambulance tayari kuwabeba walio zidiwa na pombe (hahaha).Zaidi ya hayo wapo askari wa doria ambao wanazunguka mtaani kwa magari na baiskeli, pia kwa miguu.Changamoto yetu hapa ni serikali zetu kua makini na vitendea kazi vya maafisa wetu wa kulinda usalama mahali popote nchini

(Gari la polisi aina ya Range Rover)

No comments: