11 April, 2010

kazi ni kazi tu...

Ule msemo wa kazi ni kazi na riziki ni popote ili mradi mkono uende kinywani unaji dhihirisha katika picha hii. Mimi nilidhani haya mambo ni ya ngozi nyeusi tu! kumbe hata weupe wamo!! sasa tuache ubitozi tufanye kazi!!!! Katika pita pita zangu nimegundua kufanya baadhi ya kazi ulaya kumepewa jina maarufu kama KUPIGA BOX kwa baadhi ya kazi ( kama hio kazi yako........heheheh), kwahio TUPIGE BOX kama tunataka pesa of which najua kila mtu anazitaka kwahio tupige kazi kwa bidii kama huyu mama japo kwa namna mbali mbali kutokana na nafasi zetu ili tuweze peleka mkono kinywani vitu kama Burger, wings,vodka na mbege kama ipo unaweza nunua ukiwa na pesa!!! Ulaya kila kitu pesa ati!




Fanya kazi!!!!

No comments: