04 August, 2011

HOSNI MUBARAK KUVUNA ALICHOPANDA!


Aliyekua Rais wa Misri (Egypt) Hosni Mubarak-83 ambaye alijiuzulu kufuatia maandamano makubwa kufuatia tuhuma za rushwa na uongozi wa mabavu.Mnamo April,2011 aliwekwa chini ya ulinzi bila kujali afya yake iliyozorota na jana (Jumatano Agasti 03,2011)  pamoja na hali yake kiafya kuyumba alifikishwa mahakamani kujibu mashtaka ya rushwa iliyo kithiri,kuua waandamanaji jitihada ambazo hazikuzaa matunda mpaka alipo achia ngazi mwezi Januari 2011. Wakati huo huo hali ya Misri bado tete kutokana mvurugano uliopo kati ya serikali ya sasa na waombolezaji ambao walizuiwa kuandamana ikiwa ni ishara ya kuwakumbuka watu waliopoteza maisha katika harakati za kumtoa Mubarak


Mubarak pamoja na mwanaye wamekana mashataka dhidi ya Rushwa na mauaji ya waandamanaji na kwa sasa waandamanaji wameahidi kutulia wakisubiri hukumu itolewe kwa Mubarak na vibaraka wake.Japo waliofika mahakamani waliweza wafukuza polisi kwa mawe. HII NI CHANGAMOTO KWA SERIKALI ZETU KATIKA UWAJIBIKAJI NA MATUMIZI YA NGUVU WANAPOWAKOSEA WANANCHI (WAPIGA KURA),KASHFA ZA RUSHWA NA UWAJIBISHWAJI.


Kwa habari zaidi soma HAPA,HAPA,HAPA na HAPA

No comments: