29 June, 2011

WAZIRI WA FEDHA UFARANSA AWA MKUU WA IMF

                                                                 Christine Lagarde Boss mpya wa IMF


Hatimaye aliyekua waziri wa fedha nchini ufaransa (France)  Bi Christine Lagarde, 55 awa mkuu wa IMF baada ya aliyekua mkurugenzi wa shirika hilo bwana Dominique Strauss-Kahn kujiuzulu kutokana na kashifa ya kutaka kubaka mhudumu wa hoteli nchini Marekani May 2011.


Bi Lagarde ni mwanamke pekee ambaye aliingia katika kinyang'anyiro hicho na watu wengine tisa akiwemo Mohamed El-Erian (Egypt),Stanley Fischer (Israel),Gordon Brown (UK),Kemal Dervis (Turkey),Peer Steinbrueck (Germany),Montek Singh Ahluwalia (India),Agustin Carstens (Mexico),Trevor Manuel (South Africa) na Axel Weber kutoka Ujerumani (Germany)


Kwa mujibu wa vyombo mbalimbali vya habari Bi Lagarde alichuana vikali na Agustin kutoka Mexico na hatimaye kushinda baada ya kuungwa mkono na jumuiya ya Ulaya pamoja na Marekani.Bi Lagarde anatarajia kuanza kazi rasmi kama mkurugenzi wa IMF tarehe 5 July 2011.Wanawake nao wanaweza tuwape nafasi!


Kwa habari zaidi SOMA HAPA






No comments: