11 June, 2010

Tyson wa sasa......

Je wewe ni mpenzi wa Mike Tyson, they call him 'the one and only' kutokana na record yake nzuri katika anga za boxing (aka Ngumi za kulipwa). Basi 'the one and only; ni kama lilikua jina kila kwenye mpambano lazima usikie 'the one and only'.Je wewe ni mmoja wao wa waliokua wanaamka usiku kuangalia mpambano wake? Mbaya zaidi kwakua ni usiku sana hasa kwa wale tuliokua bongo basi kabla usingizi haujaisha vizuri pambano limeisha kwa ile maarufu kama 'knock out' hii ilikua ndio style yake at the very first beginning ya mpambano wake.Ilikua inaboa kiasi fulani, je una kumbuka enzi hizo ulikua wapi? Twambie.. (LOl!)

Tukiachia mbali vurugu zake mtaani mwana masumbwi huyu amestaafu fani hio na sasa anajiita baba safi wa familia na ule wote ulikua utoto tu sasa ashakua.

Msikilize hapa:


Basi kwa wale ambao hatujamuona karibuni leo mtamuona hapa hapa The Network.Kama ilivyokua taabu kumtambua aka 50 ambaye kwa sasa amepungua kiasi cha kutisha kimuonekano.Msanii huyo maarufu toka marekani yuko bize na kusaka noti hadi kwenye movie!! Aidha hali imekua tofauti kwa Tyson ambaye sasa amekua bonge la mtu kutoka six pacs mpaka sijui niite one pac hahahahaha!

Basi ni maisha tu yana badirika kutokana na malengo kama ilivyo kwa 50 Cent ambaye ameamua kwa maksudi kupunguza uzito ili aendane na movie ya 'Things Fall Apart' ambayo imetengenezwa kwa kumbukumbu ya rafiki yake aliye kufa kwa cancer. Na katika kuuvaa uhusika wa mgonjwa wa Cancer ilibidi apunguze uzito kiasi ambacho kila mtu ameshangaa ama kuendelea kushangaa

50 Cent wa zamani:


50 Cent wa sasa baada ya kupunguza uzito:



Tyson wa sasa katika picha:


(Picha toka starpulse.com)

Na hii



Tyson wa zamani japo kwasababu zinazo julikana sitaweka pambano alilo pigwa (LOL!):


Hii pia


Ya mwisho zaidi nenda YOUTUBE!

No comments: